Pages

Thursday, July 31, 2014

MBEYA CEMENT YATOA MSAADA WA SARUJI 1000 UJENZI WA KIWANJA CHA MICHEZO CHUNYA


 Mkuu wa Wilaya ya  Chunya Mkoani Mbeya Deodatus Kinawilo akiwa amebeba mfuko wa Saruji pamoja na  Mtendaji  mkuu wa kiwanda cha Mbeya Cement Catherin Langreney wakati akipokea saada wa tani 50  zenye thamani ya Sh15milioni  kutoka kwenye kampuni hiyo kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja cha michezo kinachojengwa Wilayani humo.







Mkuu wa Wilaya Chunya Mkoani Mbeya Deodatus Kinawiro akiwa ameshikana mkono na Mtendaji mkuu wa kampuni ya saruji Mbeya (Lafarge)Catherin Langreney baada ya kukabidhiwa mifuko 1000 ya saruji sawa na  tani 50 yenye thamni ya Shilingi milioni 15 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja cha  kisasa cha michezo.




Mkuu wa Wilaya Chunya Mkoani Mbeya Deodatus Kinawiro akitoa maelekezo jinsi uwanja huo utakavyokuwa  mbele ya  Mtendaji mkuu wa kampuni ya saruji Mbeya (Lafarge)Catherin Langreney.
Mkuu wa Wilaya Chunya Mkoani Mbeya Deodatus Kinawiro akitoa taarifa  ya ujenzi wa kiwanda hicho

 Mtendaji mkuu wa kampuni ya saruji Mbeya (Lafarge)Catherin Langreney akiteta jambo na mwandishi mkongwe wa michezo George Chanda






Diwani wa kata Kiwanja akitoa salam katika hafla hiyo

 Mwenyekiti wa kijiji cha Mbugani Mungele akitoa salam katika hafla hiyo
Mkurugenzi wa biashara wa kampuni ya Lafarge Mr.Mbaga akizungumza jambo katika hafla hiyo



Jumla ya mifuko 1000 ya saruji sawa na tani 50 yenye thamani ya Sh15milioni imetolewa na Kampuni ya saruji  Mbeya (Mbeya cement) kwa serikali Wilayani Chunya  kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja cha  kisasa cha michezo Wilayani humo.

Ujenzi wa kiwanja hicho Chunya unatarajia kugharimu kiasi cha fedha Sh 8bilioni ambapo tayari ujenzi wake umeanza  wilayani ambapo Uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 50,000 pia unatarajiwa kuwa kitega uchumi  kwa halmashauri ya  wilaya ya Chunya na mkoa wa Mbeya.

Akizungumza wakati wa kukabidhi  saruji hiyo  Mtendaji  Mkuu wa   Mbeya Cement Catherine Langreney alisema kuwa kampuni yake imepokea maombi hayo kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Chunya na kukubali kuchangia saruji mifuko 1000 baada ya kugundua kuwa uwanja huo utaweza kutoa ajira kwa vijana wengi na kuendeleza michezo.

Langreney alisema kuwa  ksmpuni hiyo imekuwa ikichangia  huduma mbalimbali za kijamii kwa wananchi waliopo maeneo ya karibu na kiwanda hivyo, msaada huo ni sehemu ya huduma zao za kawaida kwa wananchi.

Aidha alisema kuwa uongozi wa kiwanda hicho unajipanga kutambulisha tekonolojia za kujenga nyumba bora kwa gharama nafuu kwa lengo la kuwasaidia wananchi wenye kipato cha chini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro alisema kuwa uwanja huo unajengwa na wananchi wenyewe kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo pendekezo la ujenzi wa uwanja huo aliliwasilisha kwenye vikao vya halmashauri na kuridhiwa na baraza la Madiwani.

Alisema katika vikao vyake, ambapo Halmashauri ya wilaya hiyo ilipendekeza kutenga Sh 70milioni  katika bajeti yake ya kila mwaka huku kila mwananchi akiwajibika kuchangia ujenzi wa uwanja huo kuanzia sh.2000 kwa kila mwaka ambapo matazamio uwanja huo unatarajia kukamilika 2016.

Alisema kuwa fursa ya kuwepo kwa uwanja huo wa kisasa itainua michezo ndani ya wilaya hiyo na mkoa wa Mbeya kwa ujumla hivyo wadau wanapaswa kujitokeza kuchangia maendeleo ya uwanja huo.

0 comments: