Pages

Tuesday, November 12, 2013

ALAZWA HOSPITALI ZAIDI YA MIKA 14




 “Nilipata ajali  ya kudongoka kutoka juu ya mti hadi chini na kuvunjika kiuno wakati nikiwa katika harakati za kuokota kuni na ndiyo sababu ya kulazwa hapa hospitalini kwa muda wa miaka 14 sasa kwa ajili y kuapata matibabu”
Hiyo ni kauli  ya Lines Mwamlima (43) mkazi wa kjji cha Igale Wilaya ya Mbeya  vijini akiwa katika hospitali ya Mission ya Mbozi  Wilaya ya Mbozi  Mkoani Mbeya  inayomilikiwa na kanisa la Moraviani jimbo la kusini Magharibi   alipiokuwa akiongea na Mwandishi wa makala haya hospitalini hapo.
Lines   ambaye ni mwanamke mjane  baada ya mume wake alifariki dunia  kwa  ajali  mwaka 1998 na kumuachia watoto wanne anasema kuwa alipata ajali ya kuanguka kutoka juu  ya mti hadi chini mwaka 1999 na kusababisha kuvunjika kiuno na kupata madhara makubwa katika uti wa mgongo.
“ilikuwa ni kawaida yangu kutoka nyumbani asubuhi na kwenda msituni kutafuta kuni kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kurudi nyumbani  salama lakini siku ile ilikuwa siku ya uchungu ambayo sitoweza  kuisahau  maishani mwangu “anasema
Anasema kuwa baada ya kufika katika msito huo uliopo mbali kidogo na nyumbani kwake alipanda juu ya mti kwa lengo la kukata  vimiti vidogo vidogo vilivyopo kwenye matawi ya mti huo ndipo alipoteleza na kuanguka chini .
“Baada ya kupata ile ajali nililia kwa uchungu na ndipo wasamalia wema waliposikia sauti  za kilio changu wakaja kuniangalia nakunikuta nimelala chini huku nikilia kwa nguvu kutokana na maumivi makali niliyokuwa nikioyapata na ndipo walipoamua kunikimbiza na kunileta hapa hospitalini”anasema
Anasema kuwa baada ya kufika hospitalini hapo alipatiwa huduma ya kwanza na kwamba baada ya vipimo  madaktari  walimpa kibali cha kwenda kutibiwa katika hospitali ya Taifa Mhimbili  kwa kuwa hospitalini  hapo  hakuna vifaa vya kuunghanisha mifupa yote ya uti wa mgongo .
“Walidai pia kuwa  nilikuwa na TB ya uti wa mgongo  na ndipo nilipoangukia hivyo wakasema kuwa hawana vifaa vya kuunganisha  mifupa ya uti wa mgongo na baada ya kukaa mwezi mmoja hapa nikapelekwa muhimbili  mwezi  Mei  1999”anasema
Anasema kuwa baada ya kufika muhimbili  alifanyiwa uchunguzi na kubaini kuwa alikuwa na TB ya uti wa mgongo ambapo walianza kumpa matibabu ya TB ya miezi  sita  “ambapo katika hospitali ya muhimbili nilikaa muda wa miezi mitano nakurudi  hapa tena kwani waliniuliza kama nina ndugu naweza kuendelea kukaa hapo  kwa mika watakayonipamgia lakini nilikataa baada ya kuona sina ndugu yoyote na sia uwezo kifedha wa kuishi jijini Dar es salaam”anasema
 Mwamlima anasema kuwa  baada kukataa alirudiswa katika hospitali hiyo ya Mbozi  Mission mwaka 2000 na kuanza kuendelea kupata matibabu madogodogo “lakini nilitokwa na vidonda kwenye makalio  na mgongoni kutokana na kulala kwa muda mrefu”anasema
Anasema kuwa alikaa hospitalimi hapo kwa muda wa miaka tisa na ndipo alipoomba kurudishwa nyumbani kwake kutokana na kuwakumbuka watoto wake ambapo madakatari wa hospitalini hapo walikubali kumrudisha nyumbani kwake.
“Baada ya  kurudi  nyumbani  hali ilikuwa ni mbaya sana na ndipo Dk Charles Mbwanji alipokuja kunitembelea  akanikuta hali yangu ni mbaya sijiwezi kwa lolote na mama yangu ni mzee hana uwezo wa kunihudumia  kwani  nilikuwa nahitaji mtu  mwenye nguvu kwa ajili ya wa kunigeuza hivyo Dk Mbwanji akanirudisha hapa hospitali “anasema
 Anasema kuwa  awali  katika hospitali hiyo walikuja madaktari Wazuingu ambao walikuwa wamfanyisha mazoezi na kufanikiwa kuweza kukaa  lakini madakakrati hao walipoondoka   hakuweza kupata huduma hiyo tena na hali yake kuendelea  kama ilivyo awali.
 Anaeleza kuwa  kwa sasa miguu yake haina nguvu,hawezi kutembea na kwamba hakuweza kupata hedhi ndani ya miaka sita na kwamba anaendelea kupata matibabu madogomadogo  katika hospitali hiyo lakini bado anahitaji  matibabu zaidi.
“Nahitaji kupata msaada wa matibabu zaidi kwani ninaamini kuna hospitali  kubwa ambazo zinawataalamu wa uti wa mgongo na kiuno  kwani mimi sina  uwezo ndugu wa kunifatia hizo hospitali wala fedha  kwani ndugu niliyebaki  naye huyu mama yangu ambaye ni mzee ambaye alikuwa ni mkulima lakini kwa sasa hana nguvu za kulimia yupo hapa hospitalini kwa ajili ya  kusaidia ninapokuwa nahitaji kupata haja kubwa na ndogo na kunipikia chakula”anasema
Akielezea hali ya mgonjwa huyo kwa sasa Dk Charles Mbwanji  anasema kuwa baada ya kupelekwa katika hospitali ya muhimbili ilibainika kuwa ugonjwa huo hauwezi kupona.
“Huyu mgonjwa hawezi kupona tena kwani ndivyo taarifa ya kutoka katika hospitali ya Taifa ya muhimbili kutokana na ajali alivyoipata hivyo amepooza kuanzia kiunoni hadi miguuni”alisema
Anasema kinachomfanya kuwepo muda mrefu katika hospitali hiyo ni kutokana na kuwepo kwa mazingira magumu nyumbani kwao na hana mtu wakumuuguza na kwamba uongozi wa hospitali hiyo ulikubaliana na kumuacha aendelee kukaa hospitalini hapo .
“Akikaa hapa hospitalini hali yake inakuwa nzuri kwani anapata matibabu kwa ukaribu na sasa kinachomsumbua ni  homa,vidonda katika sehemu ya makalio vilivyotokana na kulala kwa muda mrefu na kutumia mpira wa mkojo kwa muda mrefu na hivyo kumsababishia kupata ugonjwa wa UTI mara kwa mara na siku zake za hedhi kuwa nyingi kupita kiasi”anasema

Kwa upande wake muuguzi msaidizi wa hospitali ya Mbozi Mission Peter Kamendu  anasema  mama huyo anasumbuliwa nma tatizo la kufa kwa viungo vya mwili (Paraptegia) ambapo  ajali aliyoupata ilisababisha viungo vyake kuanzia kiunoni hadi miguuni kushindwa kufanya kazi.
“Tulimpokea huyu mama mwaka 1999 baada ya kupata ajali hiyo kama alivyooleza mwenyewe lakini  hospitali tumeona siyo vizuri kuacha akae nyumbani kwake wakati bado tatizo lake ni kubwa na anahitaji msaada wa karibu kutoka kwa wataalam”anasema
Naye  mama mzazi wa Lines  Zaituni Mgunji (80) anasema kuwa  uumia kwa mtoto wake limekuwa pigo kubwa kwakwe kwani  hana uwezo kifedha wa kumhudumia mtoto wake kwa ajili ya kupata matibabu zaidi ili kufanikiwa  kurudi katika hali yake ya zamani kutokana na umasikini aliokuwa nao.
“Hata hivyo naushukuru uongozi wa hospitali hii ya Mbozi  Mission kwa kuniruhusu kukaa hapa na mtoto wangu katika kipindi cha miaka 14 bila kutoa malipo yoyote kweli  mungu ni  ajabu kwani sijawahi kuona   wala kusikia muujiza kama huu wa hospitalia ya Mission ya Mbozi”anasema
Anasema kuwa kwa sasa hana uwezo kifedha “kwani sina uwezo wa  kulima tena nguvu zimekwisha mwanangu hivyo hata chakula naomba kwa wasamalia Wema ndiyo wananisaidia chakula kwa ajili yangu na mtoto wangu huyu mgonjwa”anasema
 Na Brandy Nelson

0 comments: