Pages

Thursday, November 14, 2013

KITUO CHA MSAADA WA KISHERIA




https://mail.google.com/mail/u/0/images/cleardot.gif
Kituo cha msaada wa kisheria na  unasihi Songwe (CHULECU) cha Wilaya ya Chunya  mkoani Mbeya,  kimeanza  mpango wa kutafsiri sheria kwa lugha  rahisi  kufuatana na mazingira husika,  ili kuijengea uwezo jamii wa kuzielewa sheria mbali mbali  ikiwa ni  pamoja na  kupunguza migogoro ya ardhi.

Kwa mujibu wa   Mkurugenzi wa kituo hicho   Bwana  Nyawili  Kalenga,  lengo la kuanzisha mpango huo ni  kuiwezesha jamii kuzijua sheria mbali mbali  za nchi  kwa kutumia lugha rahisi inayoeleweka  katika jamii husika.
Amesema kuwa kumekumekuwepo na ukiukwaji wa sheria za nchi katika maeneo mbali mbali hasa vijijini, kutokana na wananchi  wa maeneo hayo kutozijua sheria, na  baadhi ya watu kutumia uelewa wao mzuri wa sheria kwa kuwanyanyasa wenzao ambao hawazijui  na kujinufaisha  kwa masilahi yao binafsi.
Amesema  kuwa mpango huo utawasaidia wananchi hasa wa vijijini,  ambao hawaijui lugha ya kiingereza  na Kiswahili, kuzijua sheria kwa kupitia lugha yao  ambayo wanaitumia kwa wakati huo.
Amesema kuwa  mfano  sheria ya ardhi namba (4)  na (5) ya mwaka 1999, ambayo imeandikwa kwa lugha ya kiingereza, nimuhimu  kwa Wananchi wa vijijini ambao mara nyingi  imekuwa  ikitokea migogoro ya ardhi kwa wakulima na Wafugaji inayosababishwa na ukiukwaji wa sheria hiyo.
Bwana Kalenga  amefafanua kuwa endapo kama sheria hiyo ikatafsiriwa kwa lugha rahisi  kufuatana na mazingira  husika , itawasaidia  wakulima na wafugaji kujua haki zao  na pia kuepuka ukiukwaji wa sheria  ikiwa ni pamoja na kupunguza migogoro ya ardhi.
Mwisho 

Brandy Nelson

 

0 comments: