Pages

Monday, July 28, 2014

KUSHAMILI KWA WIMBI LA WIZI WA MITA ZA MAJI,MBEYA UWSA YATANGAZA BINGO

Kisima cha maji kilichopo katika ofisi za mamlaka ya maji safi na taka jiji la Mbeya.




WIMBI la Wizi wa mita za maji  umeshamili  jijini Mbeya ambapo ndani ya miezi miwili kuanzia Juni hadi Julai  zaidi ya  mita 50  zimeibiwa.imeeelezwa

Kutokana na kuwepo kwa tatizo hilo mamlaka ya maji safi na taka jiji la Mbeya(MUWASA)imetanganza bingo kwa mtu yeyote ambaye atatoa taarifa sahihi  ya mahali ambapo mita hizo zinapelekwa atapewa fedha tasilimu Sh300,000.


Akizungumza na gazeti hili Mwanasheria wa mamlaka hiyo Simon Bukuku  alisema kuwa wizi wa mita hizo ulikuwa ukitokea katika kipindi cha nyuma  kwa  kiasi kidogo, lakini uliibuka kwa kasi kubwa  mwaka 2012.

“Wimbi kubwa la wizi huu wa mita ulianza Julai 2012 hadi juni 2013 ambapo mita 256 ziliibiwa ndipo tulipoanza  kuchukua hatua mbali mbali  ikiwa ni pamoja na kufanya uchunguzi na kutoa taarifa katika jeshi la polisi”alisema 
```
Bukuku  alisema kuwa baada ya uchunguzi kufanyika walipata taarifa kuwa mita hizo zinapelekwa nchi jirani ya Malawi na kwenye vituo vya kuuzia vyuma chakavu ambapo oparesheni ilifanyika lakini hawakuweza kufanikiwa kuzipata mita hizo.


“Tulifanikiwa hadi kufika  nchini Malawi katika miji ya Kalonga,Mzuzu na Lilongwe lakini hatukuweza kufanikiwa kuzikuta kwani wenyeji walituambia kuwa hawakuwahi kuziona mita za Tanzania kwani hata wao wanaibiwa mita hizo na idaiwa kuwa zinaletwa hapa kwetu Tanzania”alisema 

Alisema kutokana na uchunguzi huo wizi huo ulipungua kwani kulikuwa hakuna matukio,lakini cha kushangaza ni kuibuka  upya kwa wimbi la wizi wa mita hizo kwa kutumia mbinu ya kunyofoa sehemu ya  katikati ya shaba ya mita hizo na kuacha chuma cha nje.

“Kwa mwaka huu hali imekuwa mbaya zaidi kwani ndani ya miezi miwili   ya Juni na Julai 2014  jumla ya mita 54 zimeibiwa na kuanzia February hadi Mei  mwaka huu mita 69 hivyo vitendo hivi vimekithiri katika jiji letu”alisema 

Alisema kuwa maeneo ambayo ndiyo yamekithiri kuibiwa mita hizo ni pamoja na kata ya Mwakibete,Ilomba na Luanda ambapo hatua mbali mbali zimeanza kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha wananchi kuhamisha mita zao kutoka nje  ya wigo na kuzifunga ndani ili kuepusha matukio ya wizi huo.

“Wakati uchunguzi zaidi unaendelea ili kubaini mita zinapelekwa wapi na zinafanyiwa nini, tunaomba ushirikiano wa karibu na wananchi kwani mita hizi zinaibiwa kuanzia majira ya saa 11:00  hadi  12:45 alfajiri”alisema 

Aidha alisema kuwa hatua zingine zilizochukuliwa na mamlaka hiyo ni pamoja kuziandikia barua za nchi  jirani cha Malawi na Zambia kuomba ushirikiano wa kuzibaini mita hizo na kupeana taarifa endapo watazikamata mita hizo. 

0 comments: