Pages

Monday, December 29, 2014

WAKULIMA 1200 WA MPUNGA WILAYA YA KYELA WAINGIA MKATABA WA KUKOPESHWA MBOLEA

 
 Baadhi  ya Wakulima wa zao la Mpunga  Wilaya ya Kyela wakiwa katika kikao cha pamoja cha kupitia mkataba wa kukopeshwa pembejeo za  kilimo na kampuni ya Mtenda Kyela Rice kwa lengo la kuwawezesha kuongeza uzalishaji wa mpunga ulio na ubora na kuweza kukubalika Sokoni.


 Mratibu wa miradi wa kampuni ya Mtenda Kyela Rice ya Mkoani Mbeya Idd Kinyaga akitoa maelezo mbele wakulima wa zao la mpunga Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya katika kikao cha pamoja na kupitia mkataba .
 Ofisa kilimo,ushirika na umwagiliaji Wilaya ya Kyela Joseph Njau akitoa maelezo kwa wakulima wa zao la mpunga wilayani humo
 Wakulima wa zao la Mpunga  wilaya ya Kyela wakiwa katika picha pamoja na  maofisa kutoka Kampuni ya Mtenda  Kyela Rice baada ya kukubaliana kuingia mkataba wa kukopeshwa pembejeo

 Moses Mwamaso akizungumza kwa niaba ya wakulima wa zao la Mpunga Wilaya ya Kyela wakati wa kupitia mkataba wa kukopeshwa  pembejeo za kilimo kutoka kwa kampuni ya Mtenda Kyela Rice
Mkurugenzi wa kampuni ya Mtenda Kyela Rice ya Mkoani Mbeya akizungumza mbele ya wakulima a ao la mpunga juu ya mkataba wa kukopesha wakulima pembejeo za kilimo


Kyela.Wakulima 1200 wa zao la Mpunga Wilaya ya Kyela  mkoani  Mbeya wameingia mkataba na Kampuni ya mtenda kyela Rice Supply kwa ajili ya kukopeshwa pembejeo za kilimo ikiwa ni pamoja na mafunzo ya kitaalam ya  kuboresha kilimo cha zao hilo.

Akizungumzia mkataba huo kwa niaba ya wakulima hao Moses Mwamaso alisema kuwa utawawezesha kupata  mbegu bora na mbolea ziatakazowasaidia kuongeza uzalishaji  na kupata mavuno mengi na yenye ubora  utakaoleta ushindani sokoni.

“Mpunga wa kyela unapendwa na watu kutoka maeneo mbali mbali lakii tatizso kubwa lililopo ni kuwa tumekuwa tukillima zao hili bila ya mbolea na hivyo kuambulia mavuno kidogo ambayo hayamsaidia mkulima kubalisha maisha yake”alisema 

Alisema kuwa  wakuima wengi wamekuwa wakitegemea mbolea ya ruzuku kutoka serikalini ambayo haitoshelezi kwa wakulima wote,hivyo mkopo huo utaweza kuwasaidia kuongeza  uzalishaji kutokana na malipo yake kufanyika baada ya mavuno.

Awali Mkurugenzi wa kampuni  hiyo  George Mtenda alisema kuwa  wakulima hao watapata mkopo kupitia vikundi vyao na kwamba  liba yake itakuwa ni asilimia tatu ambayo watarejesha pamoja na mkopo huo baada ya mavuno.

“Katika mkataba  huu  tumekubaliana kuwa  tutatoa mafunzo kwa wakulima wahusika wa mkopo huo, ya kuwazesha kulima mpunga wenye ubora, kwani katika marejesho ya mkopo wao yatakuwa ni mpunga ambao unaubora,ambapo tutapigiana hesabu   kwa  Zaidi ya bei  iliyopo sokoni kwa wakati huo ”alisema 

Mtenda alisema kuwa  ni lazima itumike Zaidi ya bei iliyopo sokoni ili kumsaidia mkulima kupata faida  na kumwezesha  kuinua kipato chake na kuboresha maisha yake kwa kuweza kumudu mahitaji yake ya kila siku ikiwa ni pamoja na kupeleka shule watoto wake 

Kwa upande wake  afisa kilimo,ushirika na umwagiliaji  Wilaya ya Kyela, Joseph Njau  alisema kuwa  kwa sasa uwezo wa  uzalishaji wa zao la mpunga  katika wilaya hiyo  ni tani 3.8 kwa hekta moja  kwa kilimo cha kutegemea mvua pekee  huku kilimo cha umwagiliaji ni tani 4.5 kwa hekta moja.

Njau alisema kuwa  kama wakulima hao watafuata  maelekezo ya mafunzo  hayo  na kuboresha kilimo cha zao hilo wataweza kuongeza uzalishaji na kufikia tani 4.5 hadi 5.5 kwa hekta na mazao yao kuwa na ubora ambao unakubalika sokoni.


0 comments: