Pages

Monday, November 25, 2013

Maadhimsho ya siku 16 za kupambana na ukatili wa kijinsia

Kitengo cha  Dawati la  jinsia wanawake na watoto cha jeshi la polisi Mkoa wa Mbeya kimebaini  vitendo vya waganga wa kienyeji  kuhusika katika kuwashawishi watoto wadogo kufanya vitedo vya kikatili kwa madai  ya kuwapatia utajiri.

Akizungumza  wakati wa kuadhimisha   siku ya 16 za kupambana na ukatili wa kijinsia Mwenyekiti  wa dawati hilo dani ya jeshi la polisi Mary Gumbo  alisema kuwa katika kuadhimisha siku hizo wamebaini mambo mbali mbali i yanayosababisha watoto wadogo kujiiingiza katika kufaya ukatili kijinsia.


“Katika siku hii tumefanikiwa kuwatembelea watoto waliopo katika mahabusu ya Mwanjelwa  ikiwa ni pamoja na kutoa msaada wa unga,sukari na sabuni ambapo tumebaini kuwepo kwa  watoto ambao wamefanya matukio mbali mbali  ya kikatili yakiwemo ya ulawiti huku wengine wakishawishiwa  na waganga wa kienyeji kufanya matukio hayo  kwa madai ya kupatiwa utajiri ”alisema 

Alisema kuwa kitendo  hicho  kinafanywa na baadhi  ya  Waganga  wa kienyeji kwa malengo ya kujipatia fedha kwani  ni udanganyifu  mkubwa na  unalenga kuwaharibia watoto wadogo maisha na hatimaye kuishia mikononi mwa sheria  na kufungwa.

“Jamii inapaswa kutambua kuwa  watoto wana haki ya kupata elimu na mahitaji mengine   ya kila siku na wanahitaji msaada mkubwa  wa malezi bora   kutoka kwa jamii inayowazunguka  na kumuona mtoto wa mwenzio ni wako hivyo tunahitaji kuwalea vizuri na siyo kuwashawishi kujiingiza katika kufanya vitendo vya ukatili”alisema 

Kwa  upande wake Afisa mfawidhi wa mahabusu  ya watoto wadogo Mwanjelwa  mkoani  Mbeya Doroth Samky kituo hicho kimekuwa kikipokea watoto kutoka katika maeneo mbali mbali na kwamba wengi wao wamekuwa wakikutwa na makosa huku wakiwa hawana wazazi.

Alisema  kuwa katika kuwanusuru watoto kujiingiza katika matukio  ya uhalifu ikiwa ni pamoja na kujihusisha na ukatili, jamii inapaswa kuelimishwa juu ya masuala ya haki za watoto,unyanyasaji  wa kijinsia, ukatili wa  watoto  na jinsi ya kuwasaidia watoto kuepukana na kujihusisha na matendo hayo.


0 comments: