Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Crispin Meela |
Imeelezwa kuwa Wakazi wa Halmashauri ya Busokole Wilaya ya
Rungwe Mkoani Mbeya wanaweza kuondokana na umasikini endapo kama watashiriki katika kutunza misitu kwa kufanya shughuli za ufugaji
wa nyuki na kupata Asali na Nta.
Akizungumza na Wenyeviti
kutoka vijiji 56 Mtendaji Kuu wa shirika la
Elimisha , Festo Sikagonamo alisema kuwa wenyeviti hao wanapaswa kufanya utambuzi wa misitu katika maeneo ya
vijiji vyote na kuyatunza na kuhifadhi ili iweze kuwasaidia katika
kuondokana na umasikini.
Alisema kuwa elimu inahitajika kwa wananchi juu ya uhifadhi na kwamba
wanawajibu wa kujadili kwa pamoja namna ya kuanzisha miradi
mbadala endelevu ambayo ni rafiki na mazingira ikiwa ni pamoja na
miradi ya kufuga nyuki kwa lengo la
kujipatia Asali na Nta
“Kwa sasa soko la Asali lipo wazi kwani ni bidhaa mbayo
inahitajika sana kwa matumizi mbali mbali ya binadamu hivyo mnapaswa kutumia nafasi mlionayo kwa kuwaelimisha wananchi
mnaowaongoza kuacha kufanya uhalibifu wa misiti na badala yake kutunza misitu hiyo kwa kufanya shughuli za
ufugaji wa nyuki”alisema
Naye
Mkuu wa Wilaya Rungwe Crispin
Meela amewataka wenyeviti hao wa vijiji kuondoa woga wakati wa kusimamia
uharibifu wa misitu iliyopo katika vijiji husika.
“Utunzaji wa misitu upo mikononi
mwenu hivyo hakikisheni mnafanya kazi hiyo bila kumwogopa mtu
yeyote yule,hawa wenzetu wanasiasa najua ni ngumu sana kulisemea hili
kwani wengi wanaogopo kuwaonya wananchi kwa kuogopa kunyimwa kura”alisema Mkuu
huyo wa wilaya.
Kwa upande wao Wenyeviti hao walisema kuwa wazee wa mila wamekuwa hawana mwamko wa
kutunza misitu kutokana na jamii kuwadharau wazee hao na
hivyo kuacha misitu kuendelea kuteketea pasipo uangalizi.
“Wazee wa mila wakithaminiwa na
vijana wanaoishi vijijini suala la utunzaji Misitu litakuwa endelevu na
hakuna mtu ambaye atajihusisha na uharibifu wa misitu hasa ya asili.”alisema Mwenyekiti
wakijiji cha Kandete Jobu Mwasipilege
Alisema kuwa kutokana na uharibifu
wa misitu uliopo hivi sasa ipo haja kwa serikali kuanza kutoa elimu kwa wazee
wa mila ili kuendelea kutunza misitu hiyo ambayo hivi sasa
imeharibiwa vibaya na vijana kutokana na shughuli za kijamii.
“Unajua ndugu zangu wenyeviti zamani
mzee wa mila alikuwa akisema jambo lilikuwa linaeleweka kwani
kutokana na nguvu za kuaminika katika jamii kuwa mzee wa mila ni kila
kitu hivyo hakuna mtu ambaye alikuwa akithubutu kujaribu kukata misitu au
kufanya uharibifu wowote kutokana na kuambiwa kuwa katika misitu hiyo
kuna nyoka mkubwa ambaye anadhulu watu hivyo kutokana na kauli hizo
hakuna kijana aliyekuwa akijaribu kufika katika misitu hiyo”alisema Mwenyekiti
huyo.
Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwela Aman Kyambinga alisema kuwa
kufuatia uharibifu huo wa misitu serikali za vijiji bado zinatakiwa
kuwaita wazee wa mila na kuwa karibu nao kutokana na kauli za wazee hao
wa mila kwa jamii kuwa na ushawishi kwa wananchi na kukubalika .
0 comments:
Post a Comment