Pages

Tuesday, December 10, 2013

Hakuna Mfumo maalum wa utoaji wa taarifa ya afya ya uzazi kwa vijana -AMREF





Mchambuzi wa Sera kutoka shirika la utafiti wa dawa na tiba (AMREF)Meshack Mollel akitoa mada juu ya uandishi wa habri za afya ua uzazi kwa vijana  kwa Waandishi wa habari na Wahariri kutoka mikoa ya Iringa,Njombe,Mbeya,Morogoro na Dar es Salaam katika  chuo cha Kilimo SUA  Morogoro.




Imeelezwa  kuwa hakuna mfumo maalum wa  upatikanaji wa taarifa za afya ya uzazi kwa vijana na kuwasababishia  kupata changamoto mbali mbali ikiwa ni pamoja na maambukizi ya virusi vya Ukimwi,mimba za utotoni na magonjwa ya zinaa.

Hayo yameelezwa na mchambuzi wa  sera katika shirika la utafiti  wa madawa na tiba (AMREF)Meshack Mollel  alipokuwa akizungumza katika semina ya siku tatu ilitolewa na shirika hilo kwa  waandishi wa habari  kuhusu   haki za afya ya uzazi kwa vijana inayofanyika katika  chuo cha kilimo SUA Mkoani  Morogoro.


Alisema kuwa  ni muhimu kwa vijana kuanzia umri wa miaka 10 hadi 24  kupata taarifa za uzazi ili kuweza kukabiliana na changamoto zinazowazunguka katika mazingira yao na kwamba  idadi kubwa  vijana ndiyo wanaoathiriwa na changamoto hizo.

 “Kwa mujibu wa Sensa ya watu ya hivi karibuni idadi kubwa ya Watanzania ni vijana hivyo jamii inapaswa kutambua  kuwa  hawa   vijana wanahaki ya kupata  afya ya uzazi ili kuwaepusha katika matatizo ambayo tumekuwa tukiyashuhudia katika maeneo yetu yanayozunguka”alisema 

Mollel alisema kuwa  kati ya wakina mama 8000 wanaokufa   kila mwaka kutokana na uzazi asilimia kubwa ya wakina mama hao ni vijana na kwamba  vijana wanachangia katika maambukizi ya mapya ya virusi vya ukimwi kwa asimilia 60.

Alisema kuwa  kuna haja kwa serikali kuona umuhimu wa uwepo wa vituo vya kutolea tarifa ya afya ya uzazi kwa vijana ili kuweza kukiokoa kizazi cha vijana ambacho  ndiyo nguvu kazi kubwa tegemeo kwa Taifa  ambacho kwa sasa kimekuwa kikiathirika kutokana na kukosa haki ya kupata taarifa afya ya uzazi.

Aidha  alisema kuwa  wakati sasa umefika kwa jamii kuondokana na mila potofu za kuzuia watoto kupata elimu  za afya ya uzazi kwa madai ya kuwa na umri mdogo huku kukiwa na matukio mengi ya mimba za utotoni.

0 comments: