Pages

Friday, December 6, 2013

Wanunuzi wa kahawa mbichi kuchukuliwa hatua kali za kisheria

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya Dk.Michael Kadeghe



Serikali  Wilayani Mbozi Mkoani Mbeya imejipanga kuwachukulia  hatua kali za kisheria makampuni yatakayobainika  yanunua kahawa mbichi (CHERRY)kutoka  kwa wakulima.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Dk.Michael  Kadeghe alipokuwa akizungumza na Wakulima na Wadau wa zao la kahawa kwenye  katika kituo cha utafiti wa kahawa (TACRI)cha  Mbimba Wilayani Mbozi.


Dr. Kadeghe  alisema kuwa ununuzi wa kahawa mbichi unamyonya mkulima  na kusababisha kuwepo kwa  matukio ya uhalifu mashambani  kwa  Wahalifu kuingia shambani na  chuma kahawa mbichi na kwenda kuuza kwenye makampuni hayo.

Aidha alisema kuwa  ununuzi wa kahawa mbichi  yanaathiri  uchumi wa Wilaya ya Mbozi  kwani   zaidi  ya  asilimia 80  ya  mapato ya Halmashauri  hiyo yanetegemea  zao la Kahawa.

Alisema  kuwa  kilimo cha kahawa  ni muhimu  katika wilaya hiyo kwani uchumi wa Wananchi unategemea  zao hilo   ambapo  kila msimu wa kahawa halmashauri hiyo inakusanya  shilingi   2.5 Bilioni.

“Utaratibu umeandaliwa wa jinsi ya kuwakamata tutakaowabaini wananunua kahawa mbichi kwani kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya  imejipanga na kuweka mikakati yake ya kuhakikisha tabia hii ya baadhi ya makampuni na watu wanataka kujinufaisha kupitia mkulima inakomeshwa”alisema 

Aidha  alisema kuwa serikali Wilaya pia imeandaa utaratibu wa kugawa bure  miche ya kahawa  kwa Wakulima ili kuwawezesha  wakulima  hasa vijana kuweza kuongeza uzalishaji wa zao la kahawa  na kuweza kuondokana katika umasikini.

“Vijana  wengi hawana shughuli za kufanya  hivyo tumeamua kama Wilaya kuhakikisha hakuna vijana wanaoshinda vijiweni  kwa kuwagawia  bure miche ya kahawa na kuwapa ruzuku ya pembejeo  ili waweze kujihusisha na kilimo cha zao la kahawa”alisema 

Akizungumza  kwa  ya Wakulima  Mtemi Miya alisema kuwa ubora wa kahawa  katika Mkoa wa Mbeya sio wa kuridhisha kwani kahawa nyingi bado iko kwenye madaraja ya chini kwani msimu mwaka 2012,2012 karibu asilimia 96.4  ya kahawa yote ilikuwa katika daraja la tisa.





Alisema  kuwa  hali hiyo  inachangia  kushusha kipato cha  Wakulima kwani kwa sasa kahawa hununuliwa na kulipwa kwa madaraja hivyo  wanaiomba  serikali  kuwasaidia Wakulima katika kuhakikisha wanazalisha kahawa yenye ubora unaotakiwa  sokoni  na kuweza kukuza kipato cha mkulima.     


0 comments: