Pages

Thursday, December 5, 2013

Wakulima wasilazimishwe kutumia Mbolea ya Minjingu - Kinana



Katibu Mkuu wa  Chama cha mapinduzi  Abdalhaman Kinana  amepiga marufuku tabia ya kuwalazimisha Wakulima kutumia mbolea  ya  Minjingu  kutokana na kuwa Wananchi wahaitaki Mbolea hiyo kwa madai kuwa haiwafai katika kilimo.

Kinana alitoa kauli hiyo jana katika mkutano wa hadhara alioufanya katika kiwanja cha shule ya msingi ya  Ruanda Nzovwe jijini Mbeya alipokuwa akikamilisha ziara ya kutelembea Wilaya za Mkoa wa Mbeya  kwa lengo la kuangalia changamoto mbali mbali zinazowakabili Wananchi.

Kinana alisema katika ziara yake amebaini matatizo manne katika Mkoa wa Mbeya ikiwa ni pamoja na soko la Mwanjelwa,Mbolea ya Minjingu , barabara  na tatizo la kukatika mara kwa mara kwa  umeme  na vifaa vinaharibika na kukatisha watu Starehe na matatizo ya madai ya Walimu.

Alisema kuwa  hakuna haja ya kuendelea kuwalazimisha Wananchi kutumia Mbolea  kwani wao ndiyo wanaojua ni mbolea ipi ambayo inawafaa katika  mazao yao  ya minjingu hivyo serikali inapaswa kuweka mbolea inayowafaa wananchi kwenye ruzuku.

“Inakuaje  Wakulima ambao  ndiyo wahusika na wapo huku vijijini ndiyo wanajua mbolea inayo faa katika mazao yao lakini mtu ambaye amekaa Dar es Salaam hafahamu masuala ya kilimo anawalazimisha wakulima kutumia Mbolea ya minjingu kama wao wanaona inafaa wabaki nayo wenyewe “alisema

Alisema  kuwa hao watu wanaowalazimisha  wakulima kutumia Mbolea ya minjingu wanamadaraka gani Serikali hadi kufikia maamuzi ambayo hayaendani na matwaka ya Wananchi”kwani  shamba,udongo,mbegu ni ni vya mkulima sasa iweje mtu mwingine aje kumlazimisha kutumia mbolea ambayo haina manufaa kwa mkulima huyo”alisema

Aidha katika mkutano huo Kinana alimtaka  Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro kutoa  majibu ya serikali kwa Wananchi kutokana na kukikataa Mbolea ya Minjingu ambapo mkuu huyo alisema kuwa  tayari serikali imetambua mmalalamiko hayo na kuyafanyia kazi.

Kandoro alisema kuwa kwa sasa serikali itaingiza Mbolea ya Dap kwenye Ruzuku ili mkulima aweze kuitumia badala ile ya minjingu na kwamba  serikali kushirikiana na wataalam na viwanda vinavyzalisha  mbolea ya minjingu  itafanya utafiti  wa kina ili kubaini matatizo ya Mbolea hiyo.




0 comments: