Pages

Thursday, December 5, 2013

Kinana afunguka awaambia Wananchi "Mtuhukumu tulio mbinguni siyo hawa chini"






Katibu  Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM)Abdulhamani  Kinana  ametubu mbele ya Umma kuwa chama hicho hakina sababu ya kukwepa lawama kwa kuwa muda mrefu kimechangia Wananchi kupata mateso na kudhulumiwa kutokana na kushindwa kuwasimamia watendaji wa serikali ambao wamekuwa wakifanya  mambo ovyo ovyo na kusababisha chama na serikali yake kuendelea kuchukiwa.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara  uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi ya Luanda Nzovwe jijini Mbeya  huku mamia ya watu waliodhuhuria mkutano huo wakimshangilia alisema kuwa kuna mambo mengi ambayo CCM imefanya vibaya ikiwa ni pamoja na kuyambia macho vitendo vya ovyo ovyo vinav yowaumiza Wananchi.


“Katika hili Wananchi naomba msiwalaumu hawa viongozi wa CCM walioko huku kwenu mtulaumu sisi tuliopo mbinguni ambao kwa mara nyingine tumeshiriki katika  kuwadhurumu na kuwanyanyasa nyie kwa ajili ya masilahi ya watu binafsi”alisema 

Alisema kuwa kuna  mashamba  na Viwanda ambavyo vimebinafsishwa na kuuzwa kwa bei  ndogo  na wawekezaji wa viwanda hivyo wamekuwa wakiwanyanyasa  Wananchi   huku wale wa  kwenye  mashamba  wakishindwa kuendeleza mashamba  hayo  na kuamua kuwakodishia Wananchi kwa gharama kubwa  lakini chama hicho  kimekikaa kimya bila kuchukua hatua yoyote.

“Mimi ninashangaa tunajisifia kuwa tumefanikiwa kujenga barabara  lakini hakuna tunachokifanya kwa hawa wananchi wewe ikiwa ni pamoja na kutoa ahadi za  ajira kwa vijana huku ni kuwaongopea  hawa vijana wetu kwani tutawapeleka wapi kama viwanda vingi vilivyobinafsishwa vimekufa na havifanyi kazi”alisema

 Kinana ambaye asilimia kubwa ya hotuba yake katika mkutano huo  alitumia kuichambua CCM  na kueleza ukweli  na uwazi  alisema kuwa  hakuna haja ya  viongozi wa CCM  na Wanachama wake kuimba nyimbo za Iena iena  CCM Namba  moja  wakati  hakuna kinachofanyika katika kuwasaidia Wananchi kutatua matatizo yao.



  “Harafu mnalalamika kuwa  wananchi hawaji kwenye mikutano waje kusikiliza nini utumbo? Wananchi hawawezi kuja  kuja kusikiliza ujinga  mnaosema na nyie kama  viongozi   mnatakiwa kuwajibika kwa wananchi na kufahamu nini mnatakiwa kufanya kwa wananchi sio kukaa na kubweteka tu”alisema Kinana

Kwa upande wake Katibu wa Itikadi na uenezi  wa chama cha mapinduzi (CCM) Nape Nauye amesema  kuwa katibu Mkuu Abdulhaman Kinana ni kiongozi wa mfano  wa kuigwa kutokana na utaratibu wake wa  kuzunguka nchi nzima na kusikiliza kero za Wananchi.

Alisema kuwa Katibu huyo tangu ameingia madarakani amekuwa akikiongoza chama hicho kwa kukaa na Wananchi wa ngazi ya chini na kusikiliza kero zao na kufuatilia utekelezaji wa Iran ya chama cha mapinduzi.

“Nakupongeza Katibu mkuu kwa kazi kubwa unayoifanya kwani ume weza hata kukaa chini na mabarozi wa nyumba kumi na kuwasikiliza kero zao na kubadilishana mawazo  hiki unachokifanya ni mfano na ndiyo   CCM ya hayati  baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere”alisema 

Naye Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya Godfrey Zambi  alisema kuwa hapo nyuma chama kilitaka ku[poteza mwelekeo kwa wananchi kutokana na kutojitokeza mbele ya Wananchi na kusikiliza kero zao.

Alisema kuwa kwa sasa chama hicho kimeamua kurudi na kuanza kusikiliza kero za Wananchi na kuyasemea  mambo ambayo  yanayowasumbua na wamekuwa wakikosa mahala pa kuyapeleka na kupatiwa ufumbuzi.

0 comments: