Pages

Thursday, December 4, 2014

MTOTO JUSTA MWASOMOLA (9)AOMBA MSAADA WA KIFEDHA KWA AJILI YA KUPATIWA MATIBABU

 Mtoto Justa Mwassomola (9)akiwa nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya alipofika katika ofisi hiyo kwa ajili ya kuomba msaada wa kifedha kwa ajili kupatiwa matibabu ya kuondoa uvimbe huo
MTOTO Justa   Mwasomola akiwa na baba yake mzazi Ephrahimu Mwasomola




RUNGWE .Mtoto Justa Mwasomola  mwenye umri wa miaka tisa mkazi wa kijiji  cha Masebe wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya  anaomba msaada wa fedha kwa ajii ya kupatiwa matibabu ya uvimbe uliopo juu ya pua nakusababisha kushindwa kuendelea na masomo.


Akizungumza  kwa uchungu  baba mzazi wa mtoto Ephrahimu  Mwasomola alisema kuwa tatizo hilo lilianza mara baada ya kuzaliwa mtoto huyo  mwaka 2005 ambapo kilikuwa  kama kiupele kidogo katikati ya jicho na jicho.

“Kijiupele  hicho kianza kuongezeka kadri anavyoendelea kukua ambapo baadae baada ya kufikisha miezi sita ndipo nilipompeleka katika hospitali ya Wilaya ya Rungwe  ya Makandana  kwa ajili ya kupatiwa matibabu”alisema 

Alisema kuwa mara baada ya kufika katika hospitali hiyo ya Wilaya Daktari alimwambia kuwa hospitali hiyo haina uwezo wa kuondoa huo uvimbe na ndipo walipomuandikia  barua  ya kwenda katika  hospitali ya Rufaa Mbeya.

“Mwaka huo huo 2005 tulipelekwa  rufaa mbeya na muuguzi wa wa hospitali ya makandana na baada ya kufika huko mtoto akafanyiwa uchunguzi ambapo madaktari  wa rufaa nao wakasema hawanauwezo wa kuondoa huu uvimbe hivyo natakiwa kwenda hospitali kubwa ya Muhimbili”alisema 

Baba huyo alieleza kuwa alikatishwa tamaa na hatua hiyo ya madktari wa rufaa mbeya kumwambia aende muhimbili kutokana na hali yake ya kifedha kuwa duni kwani hata ndugu zake alipowashirikisha suala hilo walidai kuwa pia nao hawana uwezo kifedha za kumsaidia mtoto wake kwenda Muhimbili kupatiwa matibabu.

Alisema kuwa aliamua  kurudi kijijini kwake na kuendelea na maisha mengine huku akimuacha mtoto huyo  na uvimbe huo ukiendelea kuongezeka  hadi hapo mwaka jana alipokutwa na mkuu wa Wilaya ya Rungwe  Crispin Meela  njiani akielekea shule.

“Baada ya mkuu wa Wilaya kumuona nilifikishiwa taarifa na Mwalimu wa shule ya msingi mapambano kuwa nahitajika kwa mkuu wa wilaya  ndipo nilipofanya hivyo na kufika ofisini kwake lakini sikumkuta  na nikaamua kurudi nyumbani hadi hivi juzi aliponitafuta tena  na kunitaka nifike ofisini kwake na mtoto”alisema

Akizungumzia tatizo  lake huku akitoa machozi  Mtoto Justa alisema kuwa anajisikia uchungu sana kwa kuwa na hali hiyo kwani kwa sasa hajawezi hata kwenda shule kutokana na wanafunzi wenzake kumcheka na kujiona ni tofauti na wenzake.

“Wenzangu kwa sasa wanaendelea na masomo wapo darasa la kwanza lakini mimi siwezi kwenda shule tena kwani mwaka jana nilipokuwa chekechea wenzangu walikuwa wananicheka na wengine kunishangaa wananizunguka  wengi mimi nakuwa katikati  naomba mnisaidie kuondoa hiki kitu usoni kwangu”alisema

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Crispin Meela alisema kuwa   alishitushwa na hali ya mtoto huyo baada ya kumuona njiani akiwa anaenda shule na ndipo alipoamua kumfuatilia ili kujua kama kuna matibabu yoyote ambayo amewahi kupata.

Meela alisema kuwa  mtoto huyo ameendelea kukaa na uvimbe huo nyumbani kwa muda wa mika tisa bila kupata matiabu yoyote na kwa kadri unavyoonyesha unaendelea kuongezeka  hivyo inawezekana tatizo hilo likawa kubwa hivyo ni vema  serikali na wasamalia wema wakajitokeza kumsaidia mtoto huyo aweze kufika muhimbili kwa ajili ya kupatiwa matibabu .

Alisema kuwa tangu alipoambiawa anatakiwa kwenda muhimbili ni muda wa miaka tisa sasa hivyo anahitaji kuanza kufuata taratibu upya  kuanzia hodspitali ya Wilaya hadi Rufaa ili aweze kupatiwa barua ya kwenda muhimbili.

0 comments: