Pages

Friday, November 29, 2013

Miaka 10 ya mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA tangu kuanzishwa kwake

Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Crispin Meela  akitoa hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya  siku ya kuadhimisha mika 10 ya TCRA katika ukumbi wa mtenda Sunset Hotel jijini Mbeya
 Meneja wa TCRA  kanda ya nyanda za juu kusini  akizungumza na Wadau
 Wadau wakisikiliza kwa makini  maelezo kuhusu TCRA katika kuadhimisha miaka 10 ya TCRA tangu kuanzishwa kwake
 Wadau waliohudhulia sherehe ya maadhimisho ya miaka 10 ya TCRA wakiwa katika picha ya pamoja
Kikundi cha utamaduni kikitoa burudani katika maadhimisho ya miaka 10 ya TCRA
Waandishi wa habari wakiwa kazini katika kuadhimisha miaka 10 ya TCRA

MIAKA 10 YA TCRA TANGU KUANZISHWA KWAKE

Meneja wa Mamlaka ya  Mawasiliano  Tanzania (TCRA) kanda nyanda za juu kusini  akizungumza na wadau mbali mbali wa mawasiliano katika kuadhimisha miaka kumi  ya TCRA tangu kuanzishwa  katika ukumbi wa Mtenda Sunset Hotel Soweto jijini Mbeya.Picha na Brandy Nelson





MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania kanda ya nyanda za juu kusini  imeazimisha miaka 10  tangu kuanzishwa kwake kwa kukutana na wadau  mbali mbali wa mawasiliano Mkoani  Mbeya kwa lengo la kubadlishana mawazo na kuelezea changamoto  na mafanikio katika sekta ya mawasiliano.
Akizungumza katika maadhimisho hayo meneja wa TCRA kanda ya nyanda za juu kusini Deogratius Moyo  alisema kuwa  watumiaji  wa simu za mikononi wameongezeka kutoka milioni  3.1 hadi kufikia takribani milioni 28.

Monday, November 25, 2013

Maadhimsho ya siku 16 za kupambana na ukatili wa kijinsia

Kitengo cha  Dawati la  jinsia wanawake na watoto cha jeshi la polisi Mkoa wa Mbeya kimebaini  vitendo vya waganga wa kienyeji  kuhusika katika kuwashawishi watoto wadogo kufanya vitedo vya kikatili kwa madai  ya kuwapatia utajiri.

Akizungumza  wakati wa kuadhimisha   siku ya 16 za kupambana na ukatili wa kijinsia Mwenyekiti  wa dawati hilo dani ya jeshi la polisi Mary Gumbo  alisema kuwa katika kuadhimisha siku hizo wamebaini mambo mbali mbali i yanayosababisha watoto wadogo kujiiingiza katika kufaya ukatili kijinsia.

HABARI KATIKA PICHA

Askari polisi kutoka Dawati la  jinsia Wanawake na Watoto kutoka  jeshi la polisi Mkoa wa Mbeya   wameadhimidha siku 16 za kupambana na ukatili wa kijinsia  kwa kutoa msaada wa unga,sukari na sabu  kwenye mahabusu ya watoto Wadogo iliyopo Mwanjelwa jijini mbeya .kulia aliyevaa sweta la kijivu ni Ofisa mfawidhi wa kituo hicho  Bibi Doroth Samky akitoa mkono wa shukrani kwa askari polisi  kutoka katika dawati hilo Biam Msele. 

Mkuu wa Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya  Bibi Magreth Malenga akiwa katika moja ya shamba darasa la zao Mpunga uliopandwa kwa mbegu za kisasa na kutumia mbolea mradi unaotekelezwa na kituo cha utafiti wa kilimo Uyole  katika kijiji cha Makwale Wilayani  Kyela

Mkazi na mkulima wa kijiji mlowo Wilaya ya Mbozi Mkoani  Mbeya Joseph Mwazembe akipandikiza miche ya kahawa katika shamba lake baada ya kuathiliwa na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Friday, November 22, 2013

HABARI KATIKA PICHA

 Mafunzo kwa vitendo chini ya mkufunzi Mkurugenzi wa jamii  Media Maxence Melo katika mafunzo ya uandishi wa habari za uchungu kwa kutumia blog kupitia ruzuku ya TMF
 Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini  Mkufunzi Mkurugenzi wa jamii  Media Maxence Melo
Washiriki wakisimama kwa pamoja wakielezea walichojifunza
Mkufunzi na Mhariri uzalishaji wa Habari leo Beda Msimbe akitoa mada katika mafunzo ya uandishi wa habari za  Blog

Tuesday, November 19, 2013

MITAA YA DODOMA

TAYARI KWA KUSHIRIKI MAFUNZO YA UANDISHI WA BLOG KWA RUZUKU YA TMF KWA KUBORESHA UANDISHI WA HABARI ZA KIUCHUNGUZI KWENYE BLOG

Thursday, November 14, 2013

TANGAZO KWA WAANDISHI WOTE MKOA WA MBEYA



JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA KUSHIRIKIANA NA APEC WANAENDESHA MAFUNZO KWA WAENDESHA PIKIPIKI @ BODABODA WAPATAO MIA NNE [400] KUHUSIANA NA USALAMA WAO, VYOMBO VYAO NA UTENDAJI WAO WA KAZI ZA KILA SIKU. MAFUNZO HAYO YATAFUNGWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  MNAMO TAREHE 16.11.2013 MAJIRA YA SAA 10:00HRS ASUBUHI TUNDUMA MJINI. WAANDISHI WA HABARI NA WANANCHI MNAKARIBISHWA.

Imetolewa na:
[DIWANI ATHUMANI – ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA

HAWA GHASIA AGEUKA MBOGO WILAYANI CHUNYA




Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) juzi aligeuka mbogo na kutaa kupokea taarifa ya maendeleo iliyotolewana na Kaimu MKurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya, Mbeya, Charles Mwakalila, baada ya kubainika kufichwa kwa mambo muhimu hususani takwimu sahihi za Fedha za miradi elimu, barabara na Maji.

Waziri Ghasia aligomea taarifa hiyo juzi mbele ya watumishi wa idara mbalimbali wa halmashauri hiyo wakati wa kikao baina yake na watumishi aliowakutanisha kwa lengo la kuwasikiliza kero zao na kuzijibia.

WILAYA YA CHUNYA YATAKIWA KUGAWANYWA





 Uongozi wa Mkoa wa Mbeya na Wilaya ya Chunya umeagizwa kufanya mchakato wa kuangalia namna ya kuweza kuigawa wilaya hiyo ili kupata wilaya nyingine kwa lengo la kuwasogezea huduma jirani na wananchi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Hawa Ghasia, alitoa agizo hilo juzi  baada ya kutolewa mapendekezo na Madiwani wa Halamshauri ya Chunya hiyo ya kuigawa Wilaya hiyo kwenye kikao kilichowakutanisha watumishi wa idara mbalimbali wa Halmashauri hiyo.

KITUO CHA MSAADA WA KISHERIA




https://mail.google.com/mail/u/0/images/cleardot.gif
Kituo cha msaada wa kisheria na  unasihi Songwe (CHULECU) cha Wilaya ya Chunya  mkoani Mbeya,  kimeanza  mpango wa kutafsiri sheria kwa lugha  rahisi  kufuatana na mazingira husika,  ili kuijengea uwezo jamii wa kuzielewa sheria mbali mbali  ikiwa ni  pamoja na  kupunguza migogoro ya ardhi.

Wednesday, November 13, 2013

Waihitimu wa chuo cha Kompyuta  cha  Grace wakiwa katika maandamano  kwenye sherehe za kuhitimu masomo yao

Mhitimu  wa masomo ya mapishi  katika chuo cha Grace cha jijini Mbeya  Recho  Nyambo akivishwa taji la viungo vya pilau na mama yake mzazi
hiki ni choo kinachotumika  kati ya moja ya kituo cha ukaguzi wa Skari wa usalama barabarani  mkoani mbeya

MATUKIO YA PICHA






MSULULU WA MAROLI KATIKA MPAKA WA TANZANIA NA ZAMBIA TUNDUMA 


MAFUNDI WAKIWA KAZINI WAKIPAKA RANGI BARABARA
Add caption

WIMBI LA WAHAMIAJI HARAMU TISHIO MBEYA

Wahammiaji  haramu wakipakizwa kwenye gari la Uhamiaji tayari kurudishwa makwao



Wimbi  la wahamiaji  haramu  limezidi kuwa tishio  Mkoani Mbeya ambapo  jumla ya Wahamiaji 369 wamekamatwa katika kipindi cha  miezi Sita kuanzia Januari hadi  Juni Mwaka huu 2013 akiwemo raia wa uingereza anayedaiwa kujihusisha na  vitendo vya ugaidi aliyekamatwa mpaka  Tanzania na Malawi wa Kasumulu Wilayani Kyela.
Kwa mujibu wa Afisa uhamiaji Mkoa wa Mbeya  Wilson Bambaganya  suala lawahamiaji halamu limekuwa ni tatizo kubwa wamekuwa wakitumia mpaka wa  Tanzania  Zambia  wa Tunduma Wilayani Momba  na  mpaka wa Tanzania Malawi  wa Kasumulu Wilayani Kyela na kusababisha kuwepo kwa usumbufu kwa Wananchi  na vyombo vya usalama.
Bambaganya  alisema kuwa  kati ya hao wahamiaji 269 ni raia wa Ethiopia,68Burundi ,13Jamhuri ya kidomkrasia ya Kongo, tisa kutoka Lwanda,Nane kutoka Malawi  na wawili kutoka nchini Zambia.

KIJIJI CHA SOME




“Ni miaka 50 tangu Tanganyika ipate uhuru wake mwaka 1961, lakini hatujawahi kutembelewa na kiongozi yeyote yule wa Kitaifa zaidi ya Diwani, na Afisa Mtendaji wa Kata ambao tumekuwa tukikutana nao katika shughuli za kila siku, lakini leo kwa mara ya kwanza tumeshuhudia mbunge wa Jimbo la Songwe”

Hivi ndivyo walivyaoanza kusema baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Some kilichopo katika kata ya Gua tarafa ya Kwimba wilaya ya Chunya, umbali wa kilomita zaidi ya 210 kutoka Chunya mjini ambapo Naibu Waziri wa Elimu na mafunzo ya Ufundi na Mbunge wa jimbo hilo, Philipo Mulugo alifanya ziara hivi karibuni katika kijiji hicho.


Aidha kijiji hicho cha Some kina  kaya 642 kati ya hizo 352 ni za
watu ambao hawajiwezi na 147  ndiyo wanaojiweza na  wananchi hao
wanategemea shughuli za uvuvi , ufugaji na kilimo katika kuendesha
maisha  yao.

Uvuvi

Shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa Kijiji hicho zinategemea zaidi uvuvi wa Samaki pamoja na kilimo, hata hivyo idadi ya samaki wanaovuliwa katika Ziwa rukwa inazidi kupungua  jambo ambalo limeanza kuathiri uchumi wa wakazi wa kijiji hicho.

Mmoja wa wakazi wa Kijiji hicho, John Mwala anasema  kuwa awali mtu mmoja alikuwa anaweza kuvua samaki zaidi ya 1000 kwa siku lakini kwa sasa wanavua samaki chini ya 100 hivyo ni dalili tosha kuwa samaki katika ziwa hilo hakuna.

Hata hivyo anasema hadi sasa hawajui chanzo cha kupungua kwa samaki katika ziwa hilo na kwamba wanasubiri utafiti wa wataalamu ili waweze kujua nini kifanyike ili hali ya samaki ilejee katika hali ya kawaida.

Kilimo

Anasema wakazi wa Kijiji hicho wanajishughuli kwa kiasi kidogo na kilimo cha mahindi na mbogamboga kutokana na hali ya ukame pamoja na ukosefu wa pembejeo za kilimo ikiwemo mbolea na mbegu.

Mwala anasema kuwa kutokana na mazingira yaliyopo katika kijiji hicho
ni vigumu wananchi wake kupata kwa urahisi pembejeo za kilimo na
Mbegu hivyo huwaamua kuegemea kwenye uvuvi ambao pia kwa sasa hauna
tija.

Aidha anasema kipindi cha miaka ya nyuma, wakazi wa kijij hicho walikuwa
wanalima zao la pamba  ambalo  baadae Serikali  ilizuia kilimo cha zao hilo kutokana na kuibuka kwa funza mwekundu aliyekuwa anashambulia zao hilo na kwamba hadi sasa hawajalipwa fedha zao za fidia.

Kuhusu Ufugaji anasema kuwa shughuli za ufugajji ni kidogo na kwamba
wafugaji hufuga mifugo yao na kuitunza hakuna biashara inayofanyika ya
mifugo na wakati fulani  wafugaji huama na kuenda kuishi sehemu
nyingine.

Huduma za Afya

Afisa Mtendaji wa kijiji cha Some Euzebius Mbalamwezi anasema kuwa kijiji hicho kinakabiliwa na changamoto ya ukosaji wa huduma za afya ambapo wanakijiji hulazimika kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 20 kufuata huduma za afya katika makao makuu ya kata.

Anasema ubovu wa miundombinu hususani barabara imekuwa ni kikwazo kwa magari kuweza kufika katika kijiji hicho hali inayofanya shughuli za kiuchumi na kijamii kuwa ngumu katika maisha ya kila siku hivyo msaada wa haraka unahitajika katika kuboresha miundombinu ya barabara ili kijiji kiweze kufikika kwa urahisi na kusaidia wanawake wajawazito kwenda Hospitali kwa urahisi kupata huduma za afya.


“Gari zinazoweza kufika huku ni Landcruser Hadtop  ambayo hata hivyo
hufika kwa shida sana kutokana na barabara kuwepo kwenye mlima mkubwa
wenye mawe na haijachongwa vizuri na hiyo gari ya uwindaji ambayo
mmekuja nayo nyie   ni kwa sababu  imetengezwa maalum kwa ajili ya
mazingira kama haya ya huku kwetu.”anasema

Huduma ya Maji

Mbalamwezi anasema kuwa katika kijiji hicho kuna tatizo la upatikanaji
wa huduma ya maji ambapo wananchi wanalazimika kutumia maji ya ziwa Rukwa na maji ya visima vilivyochimbwa kienyeji ambayo siyo safi na salama kwa matumizi ya binadamu.


Elimu

Kuhusu elimu anasema kuwa katika kijiji hicho kuna shule moja ya
msingi Some  ambayo pia mazingira ya kutolea elimu hiyo bado siyo
mazuri”kama unavyoona mwenyewe”anasema Mwalimu Mkuu msaidizi wa shule
hiyo ,Silas Masawe

Anasema kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 1987  na kwamba  mpaka sasa
ina vyumba vitano vya  madarasa ambapo vitatu ni mabanda yaliyojengwa
kwa miti na mabati, mawili yamejengwa kwa matofari ambapo moja wapo
halina madirisha na halijasakafiwa chini.

Mwl Masawe anasema kuwa pamoja na kuwepo kwa mazingira magumu ya
kufundishia maendeleo  ya Wanafunzi darasani yanaridhisha pamoja na
kuwepo na changamoto ya kuwepo na idadi kubwa ya mdondoko kutokana na
wanafunzi wengi kuamua kuacha shule na kukimbilia kwenye shughuli za
uvuvi.

Kiuchimi

Kupungua kwa samaki katika ziwa Rukwa hali ya ukusanyaji wa mapato
katika kijiji hicho ni mbaya na hivyo kushindwa kufanya shughuli za
maendeleo kutokana na kukosa fedha za kuendeshea miradi ya maendeleo.

Mtedanji  huyo wa kijiji anasema kuwa mapato ya kijiji hicho  kwa
asilimia kubwa yanategemea  Samaki mbapo kwa sasa samaki hao hakuna na
baadhi ya Wavuvi wameanza kuondoka na kwenda sehemu nyingine kwa ajili
ya kutafuta riziki.

Anasema kuwa kwa sasa kijiji hicho kinakusanya kuanzia shilingi
100,000 hadi 150,000 kwa mwezi fedha ambazo hazitosherezi kufanya
shughuli za miradi ya maendeleo ya kijiji.

Anafafanua kutokana na hali hiyo  maisha ya wakazi wa kijiji cha Some
ni magumu kwani kwa sasa wanakula mlo mmoja kwa siku na kwamba kwa
miradi yamendeleo wanategemea serikali na wafadhili  mbali mbali kuja
kutoa misaada kwa ajili miradi

“Tunamshukuru huyu muindaji wa  poli la   Rukwati Danny Mc  kwani
ametusaidia kwa kutupa kiasi cha shs milioni 30 ambazo tumejengea
vyumba vya madarasa viwili katka shule yetu ya Msingi ya Some  na
yamekamilika hivyo kuanzia sasa watoto wetu watahama kutoka katika madarasa
ya vibanda na kuhamia  kwenye haya madarasa tuliyofadhiliwa.”anasema

Anasema kuwa Wanaiomba Serikali kukikumbuka kijiji hicho kwa
kukitembelea mra kwa mara na kujionea maisha ya wakazi wa kijiji hicho
ikiwa ni pamoja na kuwasaidia kwa kuwaletea miradi mbali mbali ya
maendeleo kama ilivyo kwa vijiji vingine.

Mbunge

Mbunge wa jimbo la Songwe na Naibu Waziri wa Elimu na mafunzo ya
ufundi  Philipo Mulugo  anasema kuwa ameumizwa sana
mazingira ya kijiji hicho ikiwa ni pamoja na ubovu wa barabara,na
ukosefu wa kituo cha kutolea huduma ya Afya

“Nimeumia sana na hali ya barabara katika kijiji hiki cha some poleni
sana nimejionea mimi mwenyewe kwani hata gari imeshindwa kufika huku na
ndiyo maana nikalazimika kutumia hii gari maalum ya uwindaji ili
niweze kufika na kukutana na wananachi wa kijiji cha Some”anasema

Anasema kuwa kutokana na hali mbaya ya barabara anatoa kisi cha
milioni tatu na Mwindaji na mwekezaji wa poli la Rukwati pia anatoa
milioni tatu ambazo kwa pamoja zitatumika kwa jili ya kuchonga
barabara hiyo kwa kuwatumia vijana ambao ni wananchi wa kijiji hicho.

Anasema kuwa fedha hizo siyo kwa ajili ya kumtumia mkanadarasi bali
wakusanywe vijana kutoka katika kijiji hicho ambapo watachonga
barabara hiyo kwa kutumia dhana za kawaida na ndiyo watalipwa fedha
hizo zote milioni sita.

Kwa upande wa Kituo cha kutolea huduma ya Afya mbunge huyo amejitolea
kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya kuanzisha ujenzi wa
zahanati ambapo wananchi wataanza  kuchangia nguvu zao kwa kufyatua
tofari tayari kwa  kuanza ujenzi wa zahanati hiyo mwishoni mwa mwaka
huu 2011.

Amewataka Wananchi wa kijiji cha Some kujitoa na kushiriki kakamilifu
katika kutekeleza miadi ya maendelea na kuithamini  michango na
misaada wanayoletewa kwa kuitunza  ili kijiji hicho kiwezekuwa na
madiliko kwa kuwa maendeleo kama vijiji vingine.

Aidha amewataka kuanza kulima mazao mchanganyiko ya biasharana chakula
badala ya kutegemea samaki pekee ili kuweza kepukana na njaa ambayo
inaweza ikatokea wakati wowote kutokana na ziw hilo kupungua samaki .

Naibu Waziri wa elimuna mafunzo ya ufundi  ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Songwe Philip Mulugo akiwa katika kijiji cha Some kata ya Gua Wilaya ya Chunya



MATUKIO YA PICHA

usafiri  wa vijijini Wilaya ya Mbozi

Tuesday, November 12, 2013

WAGONJWA WA KIFUA KIKUU WAONGEZEKA MBEYA






Machi 24 ni siku ya maadhimisho ya ugonjwa wa kifua kikuu  ambapo watu wote duniani wameadhimisha siku hiyo  huku  Mkoa wa mbeya  ukiadhimisha  ukiwa na changamoto ya ongezeko la Wagonjwa wa kifua kikuu .

 Kifua kikuu ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na vimelea viitwavyo Mycobacterium Tuberculosis ambapo kinaambukizwa kwa njia ya hewa kutoka kwa mgonjwa mwenye kifua kkuu kwenda  kwa watu wengine.

ALAZWA HOSPITALI ZAIDI YA MIKA 14




 “Nilipata ajali  ya kudongoka kutoka juu ya mti hadi chini na kuvunjika kiuno wakati nikiwa katika harakati za kuokota kuni na ndiyo sababu ya kulazwa hapa hospitalini kwa muda wa miaka 14 sasa kwa ajili y kuapata matibabu”
Hiyo ni kauli  ya Lines Mwamlima (43) mkazi wa kjji cha Igale Wilaya ya Mbeya  vijini akiwa katika hospitali ya Mission ya Mbozi  Wilaya ya Mbozi  Mkoani Mbeya  inayomilikiwa na kanisa la Moraviani jimbo la kusini Magharibi   alipiokuwa akiongea na Mwandishi wa makala haya hospitalini hapo.

Brandy Nelson

AFARIKI DUNIA KWA KUNYWA POMBE KUPITA KIASI



AFARIKI DUNIA KWA KUNYWA POMBE  KUPITA KIASI

 Mkazi mmoja wa kijiji cha Masebe Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya  Anyimike Mwakyambo (54) amekutwa amefariki dunia ndani ya nyumba yake kwa kunywa pombe kupita kiasi.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amesema kuwa tukio hilo lilitokea Nevemba 11,2013 majira ya saa 12:45 jioni  Marehemu  huyo anadaiwa kuwa alikunywa pombe kupita kiasi bila kula chakula.

Aidha Kamanda Athumani ametoa wito kwa jamii kuacha tabia yakunywa pombe kupita kiasi kwani ni kinyume cha sheria na ni hatari kwa afya ya mtumiaji.

Na   Brandy Nelson