Pages

Saturday, May 31, 2014

MGANGA ANAYEUNGANISHA MIFUPA YA BINADAMU KWA DAWA ZA MITI SHAMBA NA WANYAMA



Pichani  ni mgonjwa  Wordson Pakyindi akitembea kwa kutumia magongo mara baada ya kuunganishwa mifupa kwa kutumia dawa za miti shamba na wanyama baada ya kupata ajali na kuvunjika mguu ,nyuma yake ni mganga wa asili aliyemtibu Anyimike Mabeja  katika kijiji cha Bwenda Wilaya ya Ileje Mkoani Mbeya.



Pichani  ni mganga wa asili anayeunganisha mifupa kwa kutumia  dawa za miti shamba na Wanyama  Anyimike Mabeja akimwangalia mgonjwa wake Wordson Pakyindi sehemu ambayo amemuunganisha mifupa kwa kutumia dawa hizo   katika kijiji cha Bwenda Wilaya hya Ileje Mkoani Mbeya.



Pichani  ni mgonjwa  Wordson Pakyindi akitembea kwa kutumia magongo mara baada ya kuunganishwa mifupa kwa kutumia dawa za miti shamba na wanyama baada ya kupata ajali na kuvunjika mguu ,nyuma yake ni mganga wa asili aliyemtibu Anyimike Mabeja  katika kijiji cha Bwenda Wilaya ya Ileje Mkoani Mbeya.

Ajali za barabarani, vipigo kwa kiasi kikubwa vimekuwa vikichangia watu wengi kupata ulemavu wa kudumu na wengine kulazimika kuondolewa kabisa viungo vyao kwa kuvikata kutokana na kuonekana kitaalamu havitaweza kutibika tena.

Tishio la kupata ulemavu limekuwa likitia hofu watu wengi kutokana na ukweli kuwa pindi mtu anapopata ulemavu, uwezo wa kufanya shughuli za kiuchumi unapungua kwa kiasi kikubwa na mtu kuanza kulazimika kwa kiwango fulani kuwa tegemezi.

MUME AUAW MKEWE KWA WIVU WA KIMAPENZI



KATIKA TUKIO LA KWANZA:

 MWANAMKE MMOJA ALIYETAMBULIKA KWA JINA LA CHRISTINA HAYOLA (35) MKAZI WA KIJIJI CHA LIWALANJE, ALIKUTWA AMEUAWA KWA KUKATWA KITU CHENYE NCHA KALI KICHWANI, KIFUANI NA MGUU WA KULIA  NA MUME  WAKE AITWAYE MUSSA NSAGAJE @ MWAULAMBO.

Wednesday, May 28, 2014

Matukio katika picha ya sherehe ya Kitchen Party ya Dida katika ukumbi wa rehema jijini Mbeya


 Bi harusi Mtarajiwa Hadija Abdi a.k.a Dida akikata keki katika sherehe ya Kitchen party yake iliyofanyika katika ukumbi wa Rehema jijini Mbeya

 Bi harusi Mtarajiwa akiingia ukumbini tayari kwa kuanza sherehe yake ya Kitchen party
 Bi harusi akiwa ameketi kwenye kiti maalum ndani ya ukumbi wa Rehema katika sherehe yake ya Kitchen Party katika ukumbi wa rehema jijini hapa

 Bi. Harusi mtarajiwa akiwa na Bw. harusi mtarajiwa Rashid Abdalah Msita "DJ Shibobo" na Mtangazaji wa Generation Fm  mara baada ya kuwasili ukumbini kwa ajili ya kutoa zawadi kwa mchumba wake mtarajiwa .
 Wanandoa watarajiwa wakionyesha mapenzi yao  ya kweli mbele wageni waalikwa
 Wageni waalikwa wakimpongeza Siwajibu a.k.a Mama Abdul kwa kazi nzuri na upendo aliouonyesha katika kuandaa Kitchen party hiyo


 Fundi maalufu wa nguo za kike jijini Mbeya Hidaya akimpongeza  Bi harusi Mtarajiwa Pembeni ni Mama mjasiliamali Tumpe Mwakaje
Mmiliki wa blog hii Brandy Nelson akiwa katika picha ya pamoja na rafiki zake wa katibu  kushoto ni Nicetha Mushi  na kulia ni Biam Mselemu
 Wajasiliamali Tumpe Mwakaje na Husma George Town wakiwa katika picha pamoja
 Pichani  ni Mama P,Anne Kanyamala na Nicetha Mushi wakifurahia sherehe kwa pamoja
 Mshehereshaji  maalufu wa Kitcheni party Mkoani Mbeya Teddy Ndoma a.k.a Mama Ndomba akiwa amekaa kwenye gauni la Bi harusi mtarajiwa
 Pichani ni familia ya Bi harusi Mtarajiwa
 Gwiji la taarabu Isha Ramadhani akimpongeza  Mama abdul
 Tumpe Mwakaje akiwa katika picha ya pamoja na Isha Ramadhani na MC Dida
 Kamati ya maandalizi ya sherehe hiyo wakipeleka Zawadi ambapo walimzawadia Bi harusi kiasi cha Sh 1.5 milioni
 Bi.harusi mtarajiwa akijumuika pamoja na wageni waalikwa katika kulisakata rumba

 Biam Mselemu akionyesha ufundi katika kucheza ikiwa ni alama ya  furaha  katika sherehe hiyo
 Wageni waalikwa wakilisakata rumba kwa furaja kubwa
 Nicetha Mushi,Mama p na Anne Kanyamala wakifurahia kwa pamoja
 Maharusi  watarajiwa wakicheza muziki mbele ya wageni waalikwa
 Biam Mselemu akionyesha pozi
 Nicetha Mushi hakuwa Nyuma katika kuonyesha umaridadi wake wa kuweka pozi

 Fundi maalufu wa nguo za kike Mkoani Mbeya Hidaya akiwa katika pozi

 Anne Kanyamala na Husna George Town wakiwa katika pozi la pamoja
 Dada wa mujini Tumpe Mwakaje akiwa katika pozi la ukweli


 Hapa furaha ilizidi kiwango

 Mama P akiwa katika pozi
 Wageni walikwa wakiwa wametulia kwenye viti vyao wakishuhudia matukio yanyoendelea katika sherehe hiyo


Bwana harusi mtarajiwa na wapambe wake wakiwa katika picha ya pamoja na Bi harusi mtarajiwa

Sunday, May 25, 2014

HABARI KATIKA PICHA ZA MATUKIO YA MISS MBEYA VIJIJINI

HABARI KATIKA PICHA ZA MATUKIO YA MISS MBEYA VIJIJINI

  Ofisa uhusiano wa nje wa kampuni ya bia(TBL) Abubakar Mansoli akimkabidhi mshindi wa mashindano ya urembo ya Miss Mbeya vijijini Atukuzwe Fabian zawadi ya seti  Kopyuta yenye thamani Sh800,000 baada ya kunyakua Taji hilo katika ukumbi wa Royal  Tughimbe Mbalizi Mbeya vijijini.Picha na brandy Nelson
 Mshindi wa  kwanza  wa Miss Mbeya vijijini aliyekaa akiwa  katika picha ya pamoja na mshindi wa pili Pendo Nelson na watatu  Neema Tadei


 Washiriki wa shindano la uremb la Miss Mbeya vijijini wakitoa burudani mbele ya wageni waalikwa katika ukumbi wa Royal Tughimbe Mbalizi Mbeya vijijini.

 Kikundi cha burudani  kutoka Mbalizi  kikionyesha show kali kama mfano wa kikundi cha THT

 Warembo wakionyesha show
 Jaji msaidizi wa mashindano ya  kumsaka  Miss Mbeya vijijini  Mary Gumbo akizungumza katika mashindano hayo


. Mkazi wa kijiji cha  Mbalizi Atukuzwe Fabiani  jana aliibuka mshindi wa Miss Mbeyavijijini baada ya kubwaga warembo wenzie 12 katika  mashindano yaliyofanyika  katika ukumbi wa Royal Tughimbe  na kujinyakulia zawadi ya seti Kompyuta yenye thamani  ya  ya Sh 800,000.

Akitangaza matokeo ya mashindano hayo  jaji mkuu wa mashindano hayo Maulid Lyoba ambaye ni afisa mauzo wa kampuni ya bia ya TBL  alisema kuwa  nafasi ya pili imechukuliwa na Pendo  Nelson ambaye alizawadiwa  meza ya kioo (Dressing table).