Pages

Saturday, October 17, 2015

SIMBA YAVUNJA MWIKO, YAICHAPA MBEYA CITY 1-0


 






LIGI kuu ya Vodacom imeendelea leo katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine ulipozikutanisha timu za Mbeya City na Simba ya Dar es salaam ambapo kwa mara ya kwanza imevunja mwiko na kuichapa Mbeya City bao 1-0.
Tangu timu ya Mbeya City ipande daraja mwaka juzi haijawahi kufungwa na Simba katika uwanja wake wa nyumbani na mara ambapo katika msimu uliopita  Simba ilifungwa nyumbani na ugenini.
Goli la kuvunja mwiko la Simba lilipatikana dakika ya 2 ya mchezo ambalo lilifungwa na Murshid Juuko kwa kichwa baada kona iliyopigwa na Mohamed Husein ambapo mpira ulitua kichwani kwa Murshid na kuusindikiza wavuni huku golikipa wa Mbeya City Juma Kaseja akichupa bila mafanikio.
Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Simba walikuwa kifua mbele kwa bao 1-0.Kipindi cha pili kwa timu ya Mbeya City kuonesha makeke langoni mwa Simba lakini washambuliaji wa timu hiyo walikosa ushirikiano na hivyo kujikuta wakishindwa kuliona lango la Simba.
Walinzi wa Simba Hassan Ramadhan, Said Hamis,Mwinyi Kazimoto, Justice Majabvi alijitahidi kuondosha hatari zilizokuwa zikielekezwa langoni mwa timu yao ambapo washambuliaji wa Mbeya City Hamad Kibopile,Christian Sembuli, Themi Felix, Geofrey Mlawa na Rafael Alpha walionekana kukwaa kizingiti.
Hadi kipyenga cha dakika tisini kinapulizwa Simba walitoka kifua mbele kwa bao 1-0.
Baadhi ya wapenzi na mashabiki wa timu ya Mbeya City wamedai kuwa kocha mpya wa Mbeya City Majao Mingange ana kazi ngumu ya kurejesha hamasa za wachezaji wake hasa baada aliyekuwa kocha wa timu hiyo Juma Mwambusi kuhamia timu ya Yanga.
Kocha Mwingange ambaye awali alikuwa akikinoa kikosi cha Ndanda ya Mtwara alisema kuwa kazi aliyonayo si kubwa sana kwa wachezaji wake na kuwa yapo marekebisho madogo ambayo yakifanyiwa kazi wachezaji hao wataonesha kabumbu safi katika michezo ijayo.(STORI/PICHA KWA HISANI RASHID MKWINDA)


Monday, October 12, 2015

LAFARGE TANZANIA YAZINDUA SARUJI MPYA TEMBO Supa Set





Dar es salaam,Ikiwa ni jitihada mahususi kuwapa saruji imara zaidi wakandarasi na wafyatuaji matofali Lafarge Tanzania imezindua chapa mpya ya saruji iitwayo “Tembo Supaset 42.5” ambayo ni imara na mahususi kwa ufyatuaji matofali, zege, majengo makubwa pamoja na miradi mikubwa ya miundombinu kama madaraja, barabara na  majukwaa ya michezo.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo leo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Lafarge Tanzania, Catherine Langreney alisema kwamba Tembo Supaset 42.5 ni saruji maalum iliyobuniwa ili kukidhi ongezeko kubwa la mahitaji ya saruji imara na inayokauka haraka katika soko la ufyatuaji matofali na zege na ujenzi mkubwa “Tembo Supaset ni matokeo ya utafiti makini uliofanywa na wataalamu wetu na imetengenezwa mahususi kukidhi mahitaji ya soko.”alisema.

Akizungumzia kuhusu maendeleo katika sekta ya ujenzi Langreney alisema kwamba kwa ujumla thamani ya sekta ya ujenzi nchini Tanzania inakadiriwa kuwa dola bilioni. Sekta hiyo ilikua kwa asilimia 7.8 mwaka 2014 na ni sawa na asilimia 8.6 ya pato la taifa ikiwa ni kutokana na ujenzi binafsi, usafirishaji na miradi mikubwa ya ujenzi. Tanzania ina idadi ya zaidi ya milioni 44 kufikia mwaka 2014 na inatarajiwa kuongezeka sambamba na ongezeko la mahitaji ya nyumba na miundombinu.”

Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa Lafarge Tanzania, Allan Chonjo alisema kuwa Tembo Supaset ambayo itauzwa kwenye soko la jumla na rejareja ikiwa katika ujazo wa kilo 50 ni saruji imara zaidi ikiwa na ubora kuliko saruji nyingine zilizopo kwenye soko kutokana na uimara pamoja na bei shindani ambazo zimepangwa na itakidhi mahitaji ya watumiaji kama vile:

  • Kuimarika mapema jambo ambalo litawaongezea tija wazalishaji bidhaa zinazotokana na zege
  • Ukaukaji wa haraka jambo litakaloyafanya matofali yaweze kuhamishika haraka na kuongeza tija wazalishaji
  • Mchanganyiko mzuri wa zege na matumizi kidogo ya maji kuimarisha.

Chonjo alisema kwamba Tembo Supaset imezinduliwa ili kukidhi mahitaji ya soko kuwa na saruji imara zaidi huku akitarajia saruji hyo kupanua soko la Lafarge Tanzania hususani kwa wafyatuaji ambao hutegemea saruji inayoimarika haraka katika kazi yao. “Mbali na uimara, faida nyingine ya Supaset ni kuweza kudumu kwa muda mrefu ikiwa na maana kwamba majengo yatakayojengwa kwa saruji hiyo yatadumu zaidi”

Alisema neno Supaset linamaanisha uimara kutokana na kukauka mapema na kukaa muda mrefu zaidi katika uimara na saruji hiyo ni sehemu ya saruji za chapa ya Tembo.


Saturday, October 3, 2015

MKUTANO WA WADAU WA HABARI NA WANAHABARI KUJADILI MUSTAKABALI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Mkuu wa Kanda Sekretarieti ya Maadili ya Uongozi wa Umma, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Erick Mbembati akizungumza na wanahabari katika kikao cha wadau wa habari kwenye ukumbi wa hoteli ya Mbeya Peak.

Kiongozi mwakilishi wa walemavu wa ngozi William Simwali akichangia katika kikao cha wadau wa habari.
Mwandishi wa habari Mwandamizi Laauden Mwambona akichangia mada katika kikao cha wadau na wanahabari.

Mwandishi wa habari na mpigapicha mkongwe Jonas Mwasumbi akichangia hoja kwenye mjadala wa kikao cha wadau wa habari na wadau kwenye ukumbi wa Hotel ya Mbeya Peak.

Mwandishi wa habari Festo Sikagonamo akisisitiza jambo kwenye kikao cha wadau na wanahabari mchana huu kwenye ukumbi wa Mbeyaa Peak Hotel




WANAHABARI na waandishi wa habari wametakiwa kujiamini na kujitathmini weledi wao katika utendaji wao wa kazi za kihabari ili kujiwekea mazingira salama wakati wa uchaguzi mkuu Oktoba 25,2015.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Kanda Sekretarieti ya Maadili ya Viomngozi wa Umma kanda ya Nyanda za Juu kusini Erick Mbembati katika kikao kilichohusisha wadau wa habari na waandishi kwenye ukumbi wa Hoteli ya Mbeya Peak Jijini Mbeya mchana huu.

Mbembati alisema kuwa waandishi kama wanataaluma wengine wanatakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ili kuiepusha nchi kuingia katika majanga ambayo yangeweza kuepukika.

Alisema pamoja na wanahabari kutakiwa kufanya kazi kwa maadili pia wamiliki wa wa vyombo ambavyo wanahabari hao wanavitumikia wanatakiwa kuthamini mchango wao ikiwa ni pamoja na kuwajali na kuiwapa stahiki zao kwa wakati.

''Waandishi wengi hawana mkataba wanafanya kazi katika wakati mgumu, wamiliki wao hawathamini mchango wao, hili linasababisha waingie katika mgogoro na hata kutumiwa na watu wasiokuwa wema kwa kuwapa rushwa'', alisema.

Mbembati alisema kuwa wino wa wanahabari unaweza kusababisha kuibuka kwa vita na umwagikaji wa damu hivyo ni vyema wakawa na tahadhari kubwa wakati wa uchaguzi mkuu Oktoba 25.

Aidha alisema wanahabari wanatakiwa kufanya kazi kwa kujituma ikiwa ni pamoja na kujiheshimu na kuheshimiana katika kazi zao na kwamba hili litachangia heshima kwa wanahabari na kuheshimiwa.