Pages

Thursday, September 8, 2016

*SERIKALI YAJIBU HOJA ZILIZOTOLEWA NA WABUNGE KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA UPATIKANAJI WA TAARIFA*

#Muswada wa Sheria ya Upatikanaji wa Taarifa utasaidia kuongeza uwajibikaji katika kutoa taarifa juu ya miradi ya maendeleo katika eneo husika.
#Sheria hii itaondoa urasimu wa utoaji wa taarifa katika ofisi za umma.
# Muswada huu unakidhi matakwa ya Katiba ya haki na wajibu kwa wananchi kupata taarifa.
#Muswada huu haukusudii kuficha taarifa zinazohitajika na mtafuta taarifa.
# Muswada huu utasaidia kuwa na utaratibu maalumu wa wananchi kupata taarifa.
# Muswada huu hauzuii haki ya mwananchi yeyote kupata taarifa kwa njia tofauti.
#Muswada huu unaongeza wigo kwa *waandishi wa habari* kwani nao wanahaki ya kupata taarifa.
#Muswada huu unalenga kupanua wigo wa upatikanaji taarifa ili kutekeleza matakwa ya Katiba.
*Imeandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO*
*Dodoma*



Friday, September 2, 2016

KUPATWA KWA JUA KWAVUTIA MAELFU WILAYANI MBARALI

 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla na Mkuu wa mkoa wa Songwe Luteni Kanali Chiku Gallawa wakiangalia Kupatwa kwa Jua eneo la Rujewa wilayani Mbarali mkoani Mbeya leo asubuhi Jua limepatwa leo kuanzia saa 4:15 hadi saa 7:00 mchana.
Mkazi wa Rujewa akiangalia kupatwa kwa jua kwa kutumia mashine ya kuchomolewa vyuma'Welding' wakati wa kupatwa kwa jua leo mchana.

Raia wa kigeni kutoka nchi za Ujerumani, Uingereza na Sweden wakitumia chombo maalumu cha kuchuja mionzi ya Jua kwa ajili ya kuangalia kupatwa kwa jua katika mji wa Rujewa wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

Hivi ndivyo kupatwa kwa jua kulivyokuwa kukionekana kwa kupitia chujio maalum la kuchuja mionzi ya jua.

Mkazi wa mjini Rujewa akiangalia kupatwa kwa jua kupitia miwani ya kuchujia mionzi ya jua leo asubuhi.

Mkuu wa wilaya ya Mbarali Reuben Mfune akizungumza wakati wa kupatwa kwa jua mjini Rujewa wilayani Mbarali.

Mbunge wa Mbarali Haroun Pirmohamed akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania(TAJATI) Christopher Nyenyembe

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari wakishuhudia kupatwa kwa jua leo a