Pages

Thursday, September 8, 2016

*SERIKALI YAJIBU HOJA ZILIZOTOLEWA NA WABUNGE KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA UPATIKANAJI WA TAARIFA*

#Muswada wa Sheria ya Upatikanaji wa Taarifa utasaidia kuongeza uwajibikaji katika kutoa taarifa juu ya miradi ya maendeleo katika eneo husika.
#Sheria hii itaondoa urasimu wa utoaji wa taarifa katika ofisi za umma.
# Muswada huu unakidhi matakwa ya Katiba ya haki na wajibu kwa wananchi kupata taarifa.
#Muswada huu haukusudii kuficha taarifa zinazohitajika na mtafuta taarifa.
# Muswada huu utasaidia kuwa na utaratibu maalumu wa wananchi kupata taarifa.
# Muswada huu hauzuii haki ya mwananchi yeyote kupata taarifa kwa njia tofauti.
#Muswada huu unaongeza wigo kwa *waandishi wa habari* kwani nao wanahaki ya kupata taarifa.
#Muswada huu unalenga kupanua wigo wa upatikanaji taarifa ili kutekeleza matakwa ya Katiba.
*Imeandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO*
*Dodoma*



0 comments: