Pages

Sunday, January 26, 2014

KANDORO AIKATAA TAARIFA YA MATUMIZI YA FEDHA ZA MIRADI


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiwa katika moja ya mikutano yake katika ziara ya siku tatu Wilaya ya Mbozi Mkoani  Mbeya



Mkuu wa Mkoa wa Mbeya   Abbas Kandoro aikataa taarifa ya matumizi ya fedha zaidi ya Sh 174 milioni za  miradi miwili ya  bwawa la maji katika kijiji cha Iyula na Msia Wilayani Mbozi  na kutoa wiki moja kwa halmashauri ya Wilaya kutoa maelezo ya sahihi ya miradi hiyo.

Katika  fedha hizo,  Sh 134 milioni zimetumika katika mradi wa  bwawa la maji  katika kijiji cha Iyula huku fedha zilizopokelewa  kutoka serikalini zikiwa Sh 250 milioni  na nyingine ni  Sh40milioni za mradi wa bwawa la maji la kijiji cha Msia ambapo fedha hizo zimetumika huku mradi ukiwa bado haujaaanza kutekelezwa.

Wakulima Mbozi walia na soko huria



Wakulima  katika kata ya Harungu Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya  wamesema kuwa kuwepo kwa soko   huria kumechangia   mfumo wa stakabadhi ya mazao ghalani kutotekelezwa na kusababisha maghala kutotumika kwa muda mrefu na kuua vyama vya ushirika. 

Thursday, January 16, 2014

Ajali yaua watu wawili na kujeruhi 23 Mbeya



 Wakazi wa mji mdogo wa Mbalizi Wilaya ya Mbeya wakiangalia gari aina ya Coaster mara baada ya kogongana na roli eneo la Mlima Mbalizi Wilaya ya Mbeya.



WATU wawili wakufa  papo hapo  jana  na wengine 23 kujeruhiwa, baada ya basi aina ya Coaster waliyokuwa wakisafiria kutoka Jijini Mbeya kuelekea Tunduma kugongwa kwa nyuma na Lori la mizigo katika eneo la mlima Mbalizi Wilaya ya Mbeya vijijjin.

Monday, January 13, 2014

Amuua kaka yake kwa kulipiza kisasi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya kamishna msaidizi mwanadmizi wa polisi Ahmed Msangi.


Watu wawili wameuawa katika matukio tofauti  Mkoani  Mbeya akiwemo mkazi wa kijiji cha Kapele  Wilaya ya Momba aliuawa kwa kuchomwa kisu mgongoni na mdogo wake kwa madai ya kulipiza kisasi baada ya kutangaza mtuhumiwa kuwa alitorosha mke wa mtu.

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHFI) watoa msaada wa vifaa tiba

Naibu Waziri wa afya na ustawi wa jamii DK Seif Rashid akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa vya Tiba kwa Mikoa ya Tanga na Mbeya katika ukumbi  Hospitali ya Mkoa wa Mbeya   



Naibu Waziri wa  afya na ustawi wa jamii   Dk Seif Rashid jana amekabidhi vifaa tiba kwa mikoa ya Tanga na Mbeya  vyenye  thamani  ya Sh989.1 milioni kwa ajili ya mradi wa mama na motto unaotekelezwa  kwa ushirikiano   na mfuko wa Taifa wa bima ya afya (NHFI) na benki ya maendeleo ya watu wa Ujerumani(KfW).

Uwanja wa soka wa Sokoine wa pili kimapato



Mwenyekiti wa chama cha Mpira  Mkoa wa Mbeya (MREFA)Elias Mwanjala  amesema kuwa uwanja wa kumbukumbu ya sokoine umekuwa ni  uwanja wa pili kimapato ukiongozwa na uwanja wa Taifa kutokana na kuwepo kwa timu ya Mbeya City.

Ukarabati wa uwanja wa Sokoine wafikia asilimia 95%



BAADA ya kusuasua  na kuzua hofu kubwa kwa wadau wa soka mkoani Mbeya,Hatimaye kazi ya kupanda nyasi ndani ya uwanja wa Sokoine imekamilika kwa asilimia 95, tayari kwa michezo ya mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Thursday, January 9, 2014

Kanisa la moravian jimbo la kusini Magharibi laingia katika mgogoro mkubwa




 KANISA la  Moravian jimbo la Kusini Magharibi  limeingia katika mgogoro mkubwa  baada ya bodi ya kanisa hilo  kumsimamisha  kazi  Mwenyekiti  wake  Mchungaji Nosigwe Buya  na kudaiwa kubadilisha vitasa vya mlango wa ofisi yake huku  mwenyekiti huyo akikaidi kusimamishwa kwake na  kuahidi kuendelea kutoa  huduma kwa waumini .

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi Mwenyekiti  huyo Mchungaji  Nosigwe Buya kuhusu kusimamishwa kwake alisema kuwa hakubaliani na hatua hiyo kwani barua aliyokabidhiwa ya kusimamishwa kwake  haikujitosheleza kutokana na kutoonyesha sababu za kusimamishwa.

Wednesday, January 8, 2014

Baadhi ya shule za msingi hazina vyoo jiji la Mbeya

 Wakati shule za msingi nchini zimefunguliwa baada ya mapumziko yamhula wa kwanza,shule mbili za msingi za Mapambano na Nero katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya hazina huduma za vyoo tangu mwaka 2012.Imeelezwa

Shule hizo za msingi ambazo zina wanafunzi zaidi ya 2600,huduma ya vyoo imekosekana kutokana na matundu ya vyoo takribani 32 yamejaa,hali inayoweza kusababisha magonjwa ya mlipuko kwa wanafunzi hao.

Thursday, January 2, 2014

Mwanamke auawa kwa kupigwa na mume wake




WATU wawili wamefariki dunia katika matukio tofauti Mkoani Mbeya akiwemo mwanamke mmoja Huruma Laiton (20) amerariki dunia  jana akiwa anapatiwaa  matibabu katika hospitali ya rufaa Mbeya baada  ya kupigwa  na mume wake kwa madai  ya kumfumania akifanya mapenzi na binamu yake ndani ya nyumba yao katika kijiji cha  Inyala Iyunga mkoani hapa.