Pages

Thursday, April 21, 2016

RC MBEYA AAGIZA KUSHUGHULIKIA WATUMISHI HEWA











 




MKUU wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla ameunda kikosi kazi cha watu 14 kilichogawanyika katika makundi mawili ambacho kitapitia upya uhakiki wa majina ya watumishi hewa na kurejea kufanya uhakiki kati ya April 20 hadi 24.

Makalla aliagiza uhakiki huo kufanyika kati ya tarehe 25 hadi 29 ambapo awali alipata taarifa ongezeko la watumishi hewa 3 katika halmashauri ya Jiji la Mbeya na watumishi 7 kutoka halmashauri ya Mbeya.

Alisema katika uhakiki wa awali  Mkoa wa Mbeya na Songwe uligungulika kuwa na watumishi hewa 94 waliosababisha hasara ya sh milioni 457 na kuwa hadi sasa kuna jumla ya watumishi hewa 10 kati ya watumishi hewa saba ambapo Halmashauri ya Mbeya ina jumla ya watumishi 23 kutoka watumishi hewa 16 waliotajwa awali.

Makalla amewataka wafanyakazi wote kufika mbele ya kamati wakiwa na barua ya mwajiri, vitambulisho na Payroll ya mwezi Machi 2016 na kuiagiza kamati mara baada ya kufanya uhakiki watakaobainika na kesi za kujibu waburuzwe mahakamani na kutakiwa kurejesha fedha zote za serikali.


Tuesday, April 5, 2016

NAPE Atembelea cha Waandishi za Habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania

WAZIRI WA HABARI UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO NAPE NNAUYE AKIWA NA BAADHI YA WANAHABARI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI ZA UTALII NA UWEKEZAJI TANZANIA TAJATI ALIPOTEMBELEA MAKAO MAKUU YA CHAMA HICHO JANA ASUBUHI

Mwenyekiti wa TAJATI Ulimboka Mwakilili akimkaribisha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Nape Nnauye alipotembelea Ofisi za TAJATI jana asubuhi

Mgodi wa makaa ya Mawe Kiwira umejaaa Figisufigisu


WAJUMBE wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini,  wamesema Mgodi wa makaa ya mawe Kiwira umejaa figisufigisu na ulikabidhiwa kwenye Shirika la Madini la Taifa (Stamico)  ukiwa kama maiti isiyo na mwenyewe.

Sunday, April 3, 2016

Mtendaji,Mwenyekiti Kitongoji cha Nsalala washikiliwa kwa tuhuma za ubadhilifu

OFISA mtendaji na Mwenyekiti wa kitongoji cha nsalala wakipandishwa kwenye gari ya polisi mara baada ya kusomwa kwa taarifa ya tume ya uchunguzi na kutuhumiwa kuhusika na uuzaji wa ardhi ya kijiji kwa Sh8.6 milioni na fedha hizo kuziweka kwenye akaunti zao binafsi.