Pages

Wednesday, January 8, 2014

Baadhi ya shule za msingi hazina vyoo jiji la Mbeya

 Wakati shule za msingi nchini zimefunguliwa baada ya mapumziko yamhula wa kwanza,shule mbili za msingi za Mapambano na Nero katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya hazina huduma za vyoo tangu mwaka 2012.Imeelezwa

Shule hizo za msingi ambazo zina wanafunzi zaidi ya 2600,huduma ya vyoo imekosekana kutokana na matundu ya vyoo takribani 32 yamejaa,hali inayoweza kusababisha magonjwa ya mlipuko kwa wanafunzi hao.


Wakizungumza na Mwandishi wa habari hizi Wanafunzi wa shule hizo ambazo zipo jirani  walisema kuwa ni kwa muda mrefu shule hizo vyoo hivyo vimejaa na kusababisha  kujisaidia maeneo ambayo siyo husika kama kwenye maeneo ya viwanja ya shule hizo.

“Hali ni mbaya ya vyoo vyetu kwani  hili tatizo ni la muda mrefu na hasa kwa sisi watoto wa kike tunapata shida mara tunapohitaji kujisaidia wakati mwingine inatulazimu kwenda kwenye nyumba za jirani kuomba msaada hali ambayo pia inatufanya kuona  mazingira magumu “alisema Marietha Yohana mwanafunzi wa shule ya msingi Nero
Naye  Mwanafunzi wa shule ya msingi Mapambano Andrew Mwaigomole alisema kuwa  mazingira ya vyoo vya shule hiyo ni mabaya hayafai kwa afya ya binadamu  kwani rahisi kupata magonjwa ya mripuko hivyo  hatua za haraka zinahitajika  katika kutatua tatizo hilo.
Akizungumzia tatizo hilo Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Nero  Gasper Lyimo alisema kuwa  kamati ya shule na serikali ya mtaa  inataarifa ya tatizo hilo na kwamba shule yake ina matundu 17 ya vyoo ambapo  yote yamejaa na kuziba.
“Watoto wanajisaidia kwa kuzibua kidogo  matundu hayo hali ambayo ni hatari kwa afya zao lakini tulitoa taarifa kwa kamati ya shule ambapo walikubaliana na wazazi kuchangia ujenzi wa vyoo hivyo”alisema
Mwenyekiti wa  kamati  ya shule  ya  Nero Joyce Mwaituka  alisema kuwa jukumu la  ujenzi wa vyoo katika shule  za msingi ni la Wazazi ,uongozi wa mitaa  miwili ya kata ya Iyela ndiyo weneyejukumu la kuhudumia shule zao
“Baada ya kupata taarifa  tulikubaliana kila mzazi achangiae Sh4,000  na  kuna zaidi ya wazazi  3,000 kwa shule zote  lakini ni Wazazi 80 pekee ndiyo waliochangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo “alisema
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Iyela two Ezekiel Mwakilasa alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kwamba mara nyingi wamekiwa wakijadili kwenye vijao na kwamba gharama ya ujenzi wa vyoo hivyo ni Sh38 milioni ambapo hadi sasa imepatikana  Sh1.6 milioni.
Aidha baadhi ya wazazi  wa kata ya Iyela wametupia lawama  kwa viongozi wa kata ya Iyela kwamba wametanguliza siasa mbele ambapo baadhi yao wamekuwa wakiwashawishi wazazi kuchangia kiwango cha Sh2,000 badala ya Sh4,000  waliyokubaliana na kusababisha kukwama kwa ujenzi wa vyoo hivyo.

0 comments: