Pages

Thursday, February 26, 2015

LIGI DARASA LA NNE YAANZA MBEYA VIJIJINI

 KULIA ni Gordon Kalulunga akifuatiwa na Christopher Nyenyembe, wakikabidhi mpira aina ya Jabulani kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Izumbwe na Ofisa Mtendaji wa kata ya Igale wilaya ya Mbeya Vijijini mkoani Mbeya jana. Zawadi hiyo imetokana na marafiki wa Kaluunga ndani ya jimbo hilo, nje ya Jimbo, mkoa na nje ya Tanzania.



MWISHO wa ligi daraja la Nne iliyoanza kutimua vumbi katika viwanja vya Izumbwe kata ya Igale wilaya ya Mbeya Vijijini jana, wachezaji wataibuka na Jezi na mipira huku vipaji vya michezo mingine vikiibuliwa.
Hayo yalisemwa na mgeni rasmi aliyefungua ligi hiyo, Gordon Kalulunga, ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari mkoani hapa.
 

  Mmoja wa marafiki wa Kalulunga, Ayas Yusuph(ASIA PRIN), akizungumza na wananchi wa kata ya Igale Mbeya Vijijini juzi.
Mratibu wa masuala ya michezo wa marafiki wa Kalulunga, Ayas Yusuph(Asia), aliwatambulisha baadhi ya marafiki walioongoza na na mwanahabari huyo ambaoni Peter Mwalulili, Akimu Mwalupindi, Frank Paskal na George Kazumba, ambao wote waliahidi kufanikisha uendeshaji wa ligi hiyo.


 Mmoja wa marafiki wa Kalulunga, George Kazumba, akizungumza na wananchi wa kata ya Igale Mbeya Vijijini juzi.

Mmoja wa marafiki wa Kalulunga, Aimu Mwalupindi, akizungumza na wananchi wa kata ya Igale Mbeya Vijijini juzi.
 
Marafiki wa Kalulunga, waliahidi pia kuwapatia mpira mmoja wanafunzi wa shule ya msingi Izumbwe, kama zawadi ya shule na kwamba kila Jumamosi watakuwa wanafanya bonaza katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo na nje ya wilaya kama walivyofanya wiki zilizopita katika uwanja wa shule ya sekondarui Mbalizi kata ya Utengule Usongwe, kwa kuhusisha michezo ya kukimbiza kuku, riadha, mpira wa pete na michezo mingine.
Gordon Kalulunga, akizungumza na wananchi wa kata ya Igale, wilaya ya Mbeya Vijijin


Alisema kutokana na kupata taarifa fupi ya mahitaji ya uendeshaji wa ligi hiyo na uhitaji wa zawadi wakati wa kufunga ligi itakayodumu kwa mwezi mmoja, atashirikiana na marafiki zake mbalimbali ili kufanikisha ligi hiyo na zawadi pia.
“Mimi sina fedha za kununulia mahitaji yanayohitajika, lakini ni na utajiri wa marafiki mkiwemo ninyi, kwasababu mmeniona ni muhimu kwenu, nimehamasika na kuwaza upya kama kauli mbiu ya marafiki wa Kalulunga, tutatimiza” alisema Kalulunga.
Alisema tayari alikuwa amewasiliana na baadhi ya marafiki zake akiwemo Mbunge wa Jimbo la Songwe, Philipo MulugonaMbungewavitimaalummkoawaMbeya, Dkt. Mary Mwanjelwa, ambao wamekubali kuchangia mahitaji hayo.

Kwa hisani ya Mtandao wa www.kalulunga.blogspot.com

0 comments: