Pages

Friday, June 20, 2014

MWANAFUNZI AUA MWANAFUNZI MWENZIE KWA KUMPIGA NA JIWE KICHWANI

Mbeya. Mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule Sekondari NzondaHaki ya jijini Mbeya na mkazi wa Nzovwe jijini hapa, amefariki dunia baada ya kupigwa na jiwe kichwani.



Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Barakaeli Masaki alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Joshua Buku (19) na kwamba ilidaiwa kuwa alipgwa jiwe kichwani na kijana mmoja aliyetajwa kwa jina la Joshua Sadi (17) mzaki wa Simike wote wa jijini Mbeya.



Kamanda Masaki alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 11:00 jioni  eneo la Shule ya Sekondari ya St, Marts iliyopo eneo la Forest Mpya, ambapo tukio hilo lilisababishwa na ugomvi baina ya marehemu na mtuhumiwa wakati walipokuwa wakicheza  mpira wa miguu ndipo mtuhumiwa akampiga kwa jiwe kichwani na kumjeruhi.



Alisema kuwa marehemu alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya Mbeya, na kwamba mtuhumiwa amekamatwa na mwili wa marehemu huyo hadi jana ulikuwa umehifadhiwa hospitalini hapo.



Awali, ilielezwa kuwa marehemu na mtuhumiwa walikuwa wakisoma shule moja lakini mtuhumiwa aliacha masomo akiwa kidato cha tatu mwaka jana.



Wakati huo huo, Kamanda Masaki alisema kuwa mfanyabiashara na mkazi wa  Chang’ombe kitongoji cha Mwagala wilayani Chunya, Steven Daison (33) alivamiwa akiwa nyumbani kwake na watu wanne na kumjeruhi kwa kumkata mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake na kisha kumpora vitu vyake vikiwemo simu na fedha taslimu.



Kwa mujibu wa Kamanda Masaki , Daisoni aliwafahamu watu hao kwa sura na kwamba tukio hilo lilitokea juzi usiku wa saa 7:00, ambapo mbali na kumkatakata kwa mapanga pia aliporwa fedha kiasi cha Sh 1,800,000  simu pamoja na vocha za simu zenye thamani ya Sh1,200,000.



Kamanda Masaki alisema kuwa kabla ya tukio hilo watu hao walifyatua risasi  hewani na ganda moja la risasi la aina ya Short Gun liliokotwa eneo hilo.



Alisema kuwa polisi wanendelea kuwasaka wahusika na tukio hilo popote walipo ili waweze kutiwa nguvuni na mwathirika na tukio hilo amepatiwa matibabu na kuruhusiwa kurejea nyumbani kwake.






0 comments: