Pages

Tuesday, February 16, 2016

NICE CATERING ILIVYOWAPONGEZA WAFANYAKAZI WAKE MJINI MOROGORO


Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Betty Mkwasa akimvisha mgolole wa heshima Mkurugenzi wa kampuni ya Nice Catering Yona Sonero  wakati wa sherehe ya kila mwaka ya kuwapongeza wafanyakazi wa kampuni hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Nashera Hotel mjini Morogoro mwishoni mwa wiki

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Nice Catering ya Jijini Dar es salaam wakiwa kwenye picha ya pamoja mbele ya kituo cha kulelea watoto yatima cha Mehayo mjini Morogoro




Mkurugenzi wa Kampuni ya Nice Catering Yona Sonero akizungumza na mmoja wa watu wenye ulemavu Jabir Mwaipaya mjini Morogoro mwishoni mwa wiki.



Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Nice Catering wakiwa kwenye kituo cha Mehayo ambako walitoa msaada mbalimbali ya vyakula,mafuta na sabuni vyenye thamani ya sh 750,000



Mkurugenzi wa kampuni ya Nice Catering Yona Sonero na MENEJA  wa kampuni ya usafirishaji ya mabasi ya Rungwe Express Bonny Mbamba yanayofanya safari kati ya Mbeya na Dar es salaam kila siku wakisikiliza ibada baada ya kutoa msaada wa vyakula kwenye kituo cha Mehayo mjini Morogoro


MC maarufu Charles Mwakipesile akifanya maombi katika kituo cha kulelea watoto cha Mehayo.

Mkurugenzi wa kampuni ya Nice Catering Yona Sonero akifuatana na Mkuu wa wilaya ya Mvomero Betty Mkwasa wakiwasili kwenye ukumbi wa Nashera Hotel mjini Morogoro wakati wa sherehe ya kuwapongeza wafanyakazi wa kampuni ya Nice Catering mwishoni mwa wiki.

Watoto  yatima na wenye ulemavu wa akili na viungo wa kituo cha Mehayo Mkoani Morogoro,mwishoni mwa wiki wamekabidhiwa  msaada wa vyakula mbali mbali na fedha tasilimu Sh750,000 kutoka kwa  Kampuni ya Nice Catering.
 Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo,Mkurugenzi wa Kampuni ya  Nice Catering,Yona Sonero alisema  sadaka kubwa inayomgusa mungu ni ya kusaidia watoto yatima kwa kuwawezesha kuishi maisha kama walivyo watoto wengine.
“Kuna wafanyabiashara wengi ambao wamejaliwa kuwa na kipato kikubwa ni vema wakatumia sehemu ya fedha zao kuwasaidia watoto hawa ili na wao waweze kuishi kama binadamu wengine.
Aidha Sonero alisema pamoja na msaada huo wa chakula anajitolea kununua baiskeli mbili za miguu mitatu kwa ajili ya watoto wenye ulemavu wa miguu.
Alisema kampuni hiyo imekuwa ikifanya hivyo kila mwaka ambao ilitanguliwa na semina elekezi kwa watumishi wake zaidi 1000 na kwamba sadaka kuu ambayo anaitoa kwa mungu ni kuwasaidia watoto hao ,ambao wanamahitaji mengi na maisha yao ni magumu kutokana na uwezo mdogo walionao watu waliojitolea kuwalea.
Kwa upande wake mlezi wa kituo cha Mehayo kilichopo mjini Morogoro Linda Ngido alisema  kituo  hicho kina jumla ya watoto 65 wenye umri wa kuanzia miaka saba hadi 42 ambao ni yatima na ulemavu wa akili na viungo ,lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya huduma ya afya kutokana na kituo hicho kushindwa kumudu gharama za matibabu mara wanapokwenda hospitalini.
“Tunaomba serikali ikitambue hiki kituo kuwa ni kazi ya kujitolea hivyo hawa watoto wapewe msamaha wa matibabu ili waweze kupata matibabu kama ilivyo kwa watu wenye uwezo na kuondokana na usumbufu ambao tunaupata katika vituo vya afya”alisema Ngido.
Alisema anashukuru kupata msaada huo kwani utawasaidia watoto hao kupata chakula cha uhakika kwani kwa mlo mmoja anatumia sh100,000 kutokana na idadi kubwa ya watoto alionao katika kituo hicho.
Aidha alisema changamoto nyingine ni  ukosefu wa maji kutokana kushindwa kulipia gharama za maji safi na taka za Moruwasa na kusababisha kutumia maji ya visima ambayo ladha yake ni ya chumvi.
Kwa upande wake mgeni rasmi kwenye sherehe hiyo Mkuu wa wilaya ya Mvomero Betty Mkwassa aliwataka wamiliki wa makampuni mbalimbali nchini kuwa na nidhamu ya kulipa kodi serikalini.
Mkwassa alisema iwapo makampuni yatajitokeza kulipa kodi bila kusukumwa na mamlaka ya mapato nchini uwezekano wa makadirio ya ukusanyaji mapato serikalini utaongezeka mara dufu.
Alisema Kampuni ya Nice Catering ni mfano wa kuigwa kutokana na kufanya shughuli zake kwa uwazi.
''Kufanya vizuri kwa kampuni hii kunatokana na uwazi wake wa shughuli mbalimbali, hii ni dalili kwamba ni walipaji kodi wazuri,''alisema Mkwassa.
Hotel ya kisasa ya Rungwe Palace iliyopo jijini Dar es salaam


Nice Catering ni kampuni tanzu inayomiliki kampuni ya mabasi ya Rungwe Express na Rungwe Hotel ya Jijini Dar es salaam



0 comments: