Pages

Wednesday, June 1, 2016

USAID YAZINDUA MRADI WA UIMARISHAJI WA MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA KWA MIKOA 13

Kaimu Mkuu wa mkoa wa Njombe Anatory Choya(wa nne kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa wilaya za mkoa wa Njombe na watendaji viongozi wa mradi wa Uimarishaji Mifumo hya Sekta za Umma jana.

Kaimu Mkuu wa mkoa wa Njombe Anatory Choya akisalimiana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Edwin Mwanzinga kabla ya uzinduzi wa mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma mjini Njombe jana.

Watendaji na viongozi wa mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma wakati wa uzinduzi wa mradi huo mjini Njombe jana.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Njonbe Anatory Choya(kulia) akiteta jambo na Kiongozi wa Uzinduzi wa mradi wa Mifumo ya Uimarishaji Sekta za Umma kwenye ukumbi wa Kyando mjini Njombe jana.

Mkurugenzi Msaidizi Usimamizi wa rasimali watu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mariam Mmbaga akitoa ufafanuzi juu ya utendaji bora wa watendaji wa Halmashauri unavyoweza kusaidia kuboresha huduma kwa umma.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anatory Choya akitamka neno la Uzinduzi wa mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma mjini Njombe jana.

Kiongozi wa Uazinduzi wa Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma Dkt. Peter Kilima akielezea azma ya mradi huo kwa Halmashauri 93 na mikoa 13 nchini.


SHIRIKA la msaada la Marekani USAID limekuja na muarobaini utakaoweza kuzisaidia Halmashauri za miji, Manispaa na Majiji kuepukana na hati chafu kwa kuanzisha mradi wa Uimarishaji wa mifumo ya Sekta za Umma PS3.
Mradi huo wa wenye gharama ya Dola milioni 62 utaanza  kutekelezwa kwenye halmashauri 93  za miko 13 ya Njombe,Iringa,Morogoro,Mbeya,Lindi,Mtwara, Rukwa, Dodoma,Kigoma,Kagera, Mwanza,Shinyanga na Mara.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo mkoani Njombe Kiongozi wa timu ya Uzinduzi wa mradi huo Dkt. Peter Kilima alisema kuwa mradi huo utazisaidia Halmashauri kujenga dhana shirikishi katika uimarisha mifumo ya sekta za utendaji kwa umma.
Alisema mradi huo wa miaka mitano umeanza Julai 2015 ambao utaendelea hadi Julai 2020 ambapo matarajio kila halmashauri katika halmashauri 93 zitafikiwa na mradi huo.
Dkt. Kilima alisema mifumo ya utekelezaji ipo katika sehemu 5 za Rasilimali watu,Rasilimali fedha,Mfumo wa TEHAMA na Tafiti Tendaji ambapo kwa sasa imeshazinduliwa katika mikoa 7 ya Iringa,Shinyanga,Dodoma,Mwanza,Mbeya, Mtwara na Rukwa.
Alisema mradi huo umbao umeandaliwa kwa kushirikiana na serikali ya Marekani na Tanzania unatekelezwa na mashirika saba yakiwemo ya Kitaifa na Kimataifa ambayo ni Abt Associates Inc ambaye ndiye mtekelezaji mkuu pamoja na watekelezaji wasaidizi.
‘’Mradi huo utaimarisha mfumo katika ngazi ya Taifa, Mkoa na Halmashauri, utahakikisha mifumo iliyopo katika ngazi ya Halmashauri inaimarishwa kupitia kitita cha afua zilizoundwa’’alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi Usimamizi wa Rasilimali watu,Ofisi ya Rais TAMISEMI, Miriam Mmbaga alisema mradi huu utatoa msaada wa kitaaluma katika ,kuimarisha mifumo iliyopo kwenye utawala wenye lengo la ushirikishwaji katika kuboresha utoaji huduma kwa jamii.

0 comments: