Pages

Monday, August 11, 2014

AMBASPO BINGWA MASHINDANO AIRTEL RISING MKOA WA MBEYA

Nahodha wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Mbaspo Academy Boaz Mwire akiwatambulisha wachezaji wenzake kwa mgeni rasmi meneja wa kanda ya nyanda za juu kusini Straton Mushi katika fainali za mashindano hayo baina ya timu hiyo ya Mbaspo Academia ambayo ilishinda kwa mabao 4 - 1 dhidi ya Elimu kutoka mbarali mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa kumbukumbu ya sokoine jiji mbeya

 Nahodha wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Mbaspo Academy Boaz Mwire akipokea Kombe la  kutoka kwa  mgeni rasmi meneja wa kanda ya nyanda za juu kusini Straton Mushi baada ya kushinda mabao 4 - 1 dhidi ya Elimu kutoka mbarali mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa kumbukumbu ya sokoine jiji mbeya kutwaa ubingwa huo kwa mara ya pili.




 Nahodha wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Mbaspo Academy Boaz Mwire akiwakabidhi wenzake Kombe  wachezaji wenzake baada ya kutwaa ubindwa kwa kushinda kwa mabao 4 - 1 dhidi ya Elimu kutoka mbarali mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa kumbukumbu ya sokoine jiji mbeya

Wachezaji 20  waliochaguli kwa ajili ya kuunda timu ya mkoa ambapo wachezaji 16  ndiyo wanahitajika wakiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa kampuni ya Airtel kanda ya nyanda za juu kusini na chama cha mpira mkoa wa mbeya



 

Meneja wa Kampuni ya Artel kanda nyanda za juu kusini Staraton Mushi akisalimiana na wachezaji wa timu ya Elimu Kutoka Wilaya ya Mbarali

 Timu ya Mbaspo Academia  ikiwa  katika picha ya pamoja na Mmikili wa timu hiyo Seleman Harubu mwenye miwani na Meneja  kampuni ya simu  Airtel kanda nyanda za juu kusini Straton Mushi baada ya kunakua Kombe la Airtel Rising
 Timu ya  vijana ya Elimu kutoka Mbarali ikiwa tayari kwa ajili ya kukaguliwa



Timu ya Mbaspo  Academy ya jijini Mbeya  imetwaa ubingwa wa mashindano ya Airtel Rissing Stars ya 2014 chini ya miaka 17 baada ya kuifunga timu ya Elimu ya Wilayani mbarali mabao 4-1 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
 
Timu  hiyo ya Mbaspo imetwaa ubingwa huo kwa mara ya pili mfululuzi ambapo mwaka jana pia ilifanikiwa kutwaa ubingwa huo kwa kuifunga timu ya  Wilayani Mbozi .

Katika mchezo huo mabao ya Mbaspo yalifungwa na Richard Basyeti dk 6,Seif Gabriel dk 13,Joseph Shibanda dk 37 na Rafael Gondwe dk 78 wakati goli la toimu ya Elimu lilifungwa na mchezaji wake Shaibu Mussa ambaye alifunga kwa penati dk ya 85.

Akizungumza wakati wa kukabidhi kombe hilo Meneja wa kampuni ya Airtel kanda nyanda za juu kusini Straton Mushi alisema kuwa lengo la mashindano hayo ni kukuza soka la vijana na kuweza kupata wachezaji wazuri 

“Mashindano haya yatakuwa endelevu ili kuhakikisha tunakuza soka la vijana na kuibua vipaji ambavyo vitaisaidia  TFF  kupata timu nzuri ya Taifa na kuleta mwamko kwa vijana kuendelea kuipenda soka”alisema 

Alisema kuwa vijana  16 waliochaguliwa katika mashindano hayo watakwenda kupambana na vijana wengine kutoka mikoa ya Ilala,Kinondoni,Temeke,Zanzibar,Mwanza  na Morogoro ambapo watachaguliwa vijana watakaounda timu ya Taifa  ya  vijana  ambayo itakwenda nchini Garbon.

Kwa  upande wake katibu wa chama cha Mpira Mkoa wa Mbeya Seleman Harubu alisema kuwa katika mashindano hayo  vijana 20  wamechaguliwa  ambapo watachujwa  na kupatikana vijana 16  watakaounda timu ya Mkoa.




0 comments: