Pages

Thursday, August 28, 2014

BWAWA LILILOJENGWA KWA SH 3.077 LABOMOKA KABLA YA KUANZA KUTUMIKA

 Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika Mhandisi Christopher Chiza akijishika kichwa baada kushuhudia mradi wa bwawa  kwa ajili ya skimu ya mwagiliaji ya Lwanyo Wilaya ya Mbarali ambayo ujenzi wake umegharimu kiasi cha  fedha  Sh3.077bilioni,kujengwa chini ya kiwango  na kusababisha  bawawa hilo kubomoka kabla ya kuanza kutumika.




 Waziri Chiza akimuuliza maswali  mhandisi Elibariki Mwendo kutoka ofisi ya umwagiliaji kanda ya Mbeya ambao ndiyo wasimizi wakuu wa miradi hiyo baada ya kushuhudia mradi huo kubomoka kutokana na kujengwa chini ya kiwango.

Mbarali.Waziri wa kilimo,chakula na ushirika Mhandisi  Christopher Chiza jana alikelwa na  madudu katika  ujenzi wa   mradi wa bwawa la Lwanyo Igurusi Wilayani mbarali  uliogharimu kiasi cha Sh3.077bilioni kujengwa kiwango cha chini na kuagiza kuundwa kwa tume maalum itakayochunguza hali hiyo atimaye hatua kali kuchukuliwa  dhidi ya wahusika 

Mradi wa ujenzi wa bwawa hilo ulianza kutekelezwa Machi 2010 chini ya ofisi ya  umwagiliaji kanda  kwa kupata fedha kupitia mfuko wa kuendeleza kilimo cha umwagiliaji Taifa (NIDF)na kujengwa na kampuni ya Boimanda Modern Construction na kukamilisha kazi hiyo kwa mujibu wa mkataba Desemba 2013 ambapo zaidi ya wananchi 6000 walitarajia kunufaika na mradai huo.

Akizungumza baada ya kufika katika bwawa hilo alisema kuwa kutokana na hali hiyo mbaya serikali  imepata hasara kubwa  kwani mradi huo hauwezi kutumika na kwamba itachukua hatua ya kutuma  timu ya wataalam kuja kufanya uchunguzi na ukaguzi wa kitaalam(Technical Oditing) na kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika.

“Hii hali ni mbaya inaumiza kila mtu atakayefika hapa na kuona kilichofanyika nilazima aumie hivyo hakuna atakayekubaliana na hili  kwani fedha nyingi zimeteketea hapa na bwawa hili haliwezi kutumika hivyo  ni lazima watu wawajibike hapa hata kama waliohusika wamestaafu lakini serikali haistaafu hivyo itawafuata huko huko walipo”alisema

Alisema kuwa kazi itakayofanywa na timu hiyo ni kuhakikisha wanaangalia michoro ya ujenzi wa mradi huo, utaratibu uliotumika kumpata mkandarasi,jinsi malipo yalivyofanyika na kukagua uwezo wa mkandarasi.

“Nilazima huyu mkandarasi akaguliwe hivyo kwani sina imani na uwezo wake hivyo naagiza wataalam kutoka bodi ya wakandarasi (CRB) kuhakikisha wanamkagua mkandarasi huyu kwani alichotufanyia hapa ni hasara kubwa kwa serikali lakini pia nikuwanyika wananchi wetu haki ya kupata maji kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na matumizi ya nyumbani”alisema  

 Akijibu maswali ya Waziri mkurugenzi wa kampuni hiyo ya ukanadarasi ya Boimanda, Nicholaus Mgaya alisema kuwa kampuni yake ipo daraja la tatu  na kwamba mkataba wake umekwisha na alipoomba kuongezewa fedha zingine kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo alikataliwa na wahusika.

Naye  Mhandisi kutoka ofisi ya umwagiliaji kanda Elibariki Mwendo alisema kuwa  waligundua tatizo hilo la ujenzi chini ya kiwango baada ya   ujezi huo kubomoka wakati tayari mkandarasi ameshamaliza mkataba wake na fedha zote ameshalipwa.

Alisema kuwa tatizo lililopo hapo ni maji kupita sehemu  siyo sahihi  na kusababisha ujenzi wa tuta hilo kubomoka na kwamba suala la kumtafuta mkandarasi lilifanywa na halmashauri ya Wilaya ya Mbarali.

Awali akitoa taarifa kwa Waziri, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro alisema kinachomsikitisha  ni namna miradi  inayosimamiwa na ofisi  ya umwagiliaji kanada kujengwa chini ya kiwango.

”Hali hii ni mbaya sana kwa serikali yetu kwani wananchi hawawezi kutuelewa fedha nyingi mabilioni ya shilingi kupotea bure  na ujenzi wake unasikitisha  kwani utaalam unanipa mashaka “alisema 

0 comments: