Pages

Monday, August 11, 2014

MAELFU YA WATU WASHONANA KATIKA BANDA LA COCACOLA KUMSHUHUDIA IZZO B

 Msanii wa bongo fleva IZZO B akitumbuiza katika banda la Cocacola Kwanza siku ya nanenane katika viwanja vya nanenane kanda ya nyanda za juu kusuni jijini mbeya
 IZZO B akiimba kwa hisia wimbo wake wa tumoghele huku akishangiliwa maelfu ya watu waliojitokeza kumshudia katika banda la Cocacola kwanza katika viwanja vya maonyesho ya nanenane jijini Mbeya


 Meneja  mauzo kanda yanda za juu kusini Rashidi Mgonja akimkabidhi pikipiki kiongozi wa timu ya Uyole baada ya kutwaa kombe la mashindano ya bodaboda Cup yaliyoandaliwa City  Sign Ptomotion ya jiji mbeya

 Watoto wakitoa burudani kabla ya kupanda IZZO B jukwaani na kuanza kutumbuiza




Maelfu ya watu kutoka  mikoa ya kanda ya nyanda za juu kusini walijitokeza jana  kumshuhudia Msanii wa tasinia ya muziki wa bongo fleva  Izzo B  viwanja vya maonyesho ya nanenane jijini Mbeya.

Msanii huyo  ambaye yupo mbeya kwa ajili ya onyesho la Kilimanjari music  tour  linatotarjiwa kufanyika  jijini Mbeya ,jana aliibuka ghafla jukwaani katika banda la maonyesho la  kampuni yaCocacola na kuanza kuimba.

Baada ya msanii huyo kupanda jukwaani na kuanza kuimba mashabiki na wapenzi wa muziki huo waliokuwa katika mabanda mbali mbali katika viwanja hivyo walisogea kwa kasi kubwa katika banda hilo na kuanza kusukumana huku wengine wakiwa na shauku ya kutaka kumshika mkono.

Furaha ya watu iliyoongezeka pale tu msanii huyo alipoimba wimbo wake unaoitwa “Tumoghele” ambao ni wa lugha ya kabila la Wanyakyusa na  “Naongea na  Ridhiwani” kulazimika kushangilia kwa  kupiga kelele ambazo zilivuta watu wengine zaidi waliokuwepo katika viwanja hivyo vya maonyesho.

Akizungumza mara baada ya kumaliza kuimba Izzo B alisema kuwa  kutokana na kuwa ni mzawa wa Mbeya aliguswa kufika katika viwanja hivyo mara baada ya kampuni ya Cocacola  kumu mara tu baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Songwe akitoa jijini  Dar Salaam.

“Mimi ni mtoto wa hapa Mbeya nawapenda watu wote wa mbeya hivyo nasikia furaha kuwa nyumbani na daima siwezi kuwazarau kwani napenda amani na ninawaombea muendelee kuishi kwa amani na upendo”alisema
Mwisho

0 comments: