Pages

Thursday, August 14, 2014

MJUMBE WA NEC SHITAMBALA APANDISHWA KIZIMBANI



Pichani ni Mjumbe wa halmashauri kuu ya  CCM Taifa (NEC) na Wakakili wa kujitegemea Sambwee Shitambala(wa kwanza kulia)  akifurahia jambo na wakili anayemtetea Tasco Luambano  mara baada ya kufikishwa  katika mahakama ya hakimu mkazi Wilaya ya Mbeya kwa shitaka la kuingia kwa  jinai na kujenga nyumba katika viwanja viwili eneo la Gombe Uyole jijini Mbeya mali ya Jaswinder Palsigh.




Mjumbe wa halmashauri kuu ya  CCM Taifa (NEC) na Wakakili wa kujitegemea Sambwee Shitambala jana amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Wilaya ya Mbeya kwa shitaka la kuingia kwa  jinai na kujenga nyumba.


Mwendesha mashitaka wakili wa serikali Ahmed Stambuli alieleza mbele ya hakimu mkazi Wilaya ya Mbeya Gilbert Ndeuruo alisema kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo kati  Juni 18,2012 na Novemba 28,2013  katika eneo la Gombe Wilaya ya Mbeya mjini.

Alisema kuwa mshitakiwa aliingia kwa jinai katika viwanja viwili namba 27 na 28 block BB  na kujenga nyumba  kinyume na kanuni  kifungu cha kanuni ya adhamu sura  ya 16 ,mali ya Jaswinder Palsigh na kumsababishia mlalamikaji maudhi.

Mshitakiwa alikana shitaka hilo na  mwendesha mashitaka alieleza mahakamani hapo kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika  na  kwamba upande wa mashitaka hauna kipingamizi cha dhamana dhidi ya mshitakiwa.

 Ndeuruo alieleza mahakamani hapo kuwa dhamana ipo wazi kwa mshitakiwa kuwa na mdhamini mmoja na kusaini bondi ya Sh1milioni ambapo mshitakiwa alitimiza masharti hayo ya dhamana na kesi itakuwa Septemba 10,mwaka huu kwa ajili ya kusikiliza maelezo ya awali.

Akizungumza nje ya  mahakama Wakiri anayemtetea mshitakiwa huyo Tasco Luambano alisema kuwa anashangazwa  na kitendo cha kesi ya mteja wake kusikilizwa katika mahakama ya Wilaya badala ya ardhi .

Aidha alisema kuwa kesi hiyo inawahusu watu zaidi ya 400 “lakini cha kushangaza ni mteja wangu pekee ndiye aliyefikishwa mahakamni hapa lazima kuna kitu ndani yake kwani eneo analodaiwa mteja wangu kuingia kwa jinai lina nyumba za watu zaidi ya 400 ambao wanaishi katika eneo hilo la viwanja vyote viwili”alisema 

“Mteja wangu alikamatwa jana na jeshi la polisi akiwa na watu wengine wanne ambapo wote kwa pamoja walipewa dhamana na kutakiwa  kufika hapa  mahakamani kwa ajili kusomewa mashitaka yao lakini cha ajabu  wote wamefika lakini  kasomewa peke yake”



0 comments: